LIVE STREAM ADS

Header Ads

Mapokezi ya Mwenge wa Uhuru Jijini Mwanza yafana

Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.

Mwenge wa Uhuru umewasili katika Halmashauri ya Jiji la Mwanza ukitokea katika Halmashauri ya Buchosa wilayani Sengerema kwa ajili ya kukagua, kuweka mawe ya msingi na kuzindua miradi mbalimbali ya maendeleo.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG

Mwenge wa Uhuru umewasili katika Halmashauri ya Jiji la Mwanza ukitokea katika Halmashauri ya Buchosa wilayani Sengerema kwa ajili ya kukagua, kuweka mawe ya msingi na kuzindua miradi mbalimbali ya maendeleo.


Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza Mhe. Dkt. Philis Nyimbi amepokea Mwenge huo kutoka kwa Mkuu wa Wilaya Sengerema Mhe. Mwl. Emmanuel Kipole na kubainisha kwamba miradi itakayopiwa na mbio za Mwenge ina thamani ya shilingi bilioni 4.8.

Mapokezi hayo yamefanyika mapema leo Agosti 31, 2018 katika eneo la Kamanga Feri ambapo Kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa Ndg. Charles Francis Kabeho ametumia fursa hiyo kuwahimiza wazazi na walezi kutimiza wajibu wao kwa kuwapa mahitaji muhimu ya shule watoto wao katika kipindi hiki ambacho serikali inatekeleza mpango wa elimu bure ili kuwawezesha kupata elimu bora.

Aidha ameonya kuhusu suala la dawa za kulevya kwa vijana ambapo amewataka kujiepusha na matumizi ya dawa za kulevya kwa kuwa yanahatarisha maendeleo ya taifa na kuwahimiza kuwa wazalendo.

Baada ya makabidhiano hayo, Mwenge wa Uhuru umeelekea Kata ya Isamilo na kuweka jiwe la msingi kwenye ujenzi wa barabara ya Isamilo-Nyashana-Jeshini inayojengwa kwa kiwango cha mawe yenye urefu wa kilomita moja kabla ya kuwasili katika eneo la Soko Kuu katikati ya Jiji la Mwanza ili kukagua shughuli za kiuchumi za vikundi vya vijana na akinana pamoja na kukabidhi hundi ya shilingi milioni 200 kwa vikundi 52 vya wajasiriamali vya akina mama na vijana.

Shughuli nyingine zitakazofanywa na Mwenge ni pamoja na uzinduzi wa mradi wa mfumo rahisi wa maji taka katika maeneo ya miinuko uliopo Kata ya Igogo, kutembelea soko la kisasa la Igogo, kukagua duka la kisasa la usambazaji wa pembejeo za kilimo la Twiga Chemical Industrial lililopo Kata ya Mkuyuni, kuweka jiwe la msingi kwenye mradi wa umeme wa jua katika hospitali ya wilaya Nyamagana iliyopo Butimba.

Pia mwenge utazindua Klabu ya kupambana na rushwa katika shule ya msingi Nyakato B, kufungua Zahanati ya Isebanda Kata ya Lwanhima, kukagua shughuli za udhubiti ugonjwa wa Malaria Kata ya Lwanhima, kugawa kadi za kupata matibabu kwa wazee Kata ya Lwanhima na kukagua zoezi la upimaji Saratani ya shingo ya matiti Kata ya Lwanhima na kufungua shule ya msingi Buhongwa B Kata ya Buhongwa.

Baada ya shughuli hizo, Mwenge wa Uhuru utaelekea eneo la mkesha katika eneo la shule ya msingi Buhongwa B ambapo utafanyika ukaguzi wa mabanda ya maonesho ya bidhaa na huduma mbalimbali, kusoma risala ya utii ambapo kesho Septemba Mosi, 2018 utakabidhiwa katika wilaya ya Ilemela ambapo makabidhiano hayo yatafanyika katika viwanja vya Mwatex.
Mwenge wa Uhuru wakagua miradi kabambe Misungwi
Tazama BMG Online Tv hapo chini

No comments:

Powered by Blogger.