LIVE STREAM ADS

Header Ads

Raia wa kigeni wakamatwa mgodini, wengine walikuwa wamefichwa chooni

Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.

Wafanyakazi wanane raia wa kigeni wamekamatwa kwa tuhuma za kufanya kazi nchini bila vibali katika mgodi wa dhahabu wa MMG unaomilikiwa na wawekezaji kutoka nchi za Armenia na Urusi uliopo katika Kijiji cha Seka Wilaya ya Musoma mkoani Mara.

Wafanyakazi hao kutoka Urusi na Armenia wamekamatwa jana wakiwa wamejifungia katika vyumba wanavyolala kufuatia ziara ya Naibu wa Waziri wa Madini Doto Bitendo aliyoifanya mgodini hapo, huku wafanyakazi na vibarua wazawa zaidi ya 20 wakikutwa wamefichwa chooni.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Mmoja wa raia wa kigeni aliyekutwa amelala
Mmoja wa raia wa kigeni aliyekuwa amefichwa chumbani
Raia wa kigeni aliyekutwa chumbani amejifungia
Mkuu wa Wilaya ya Msoma ameagiza hatua za kisheria kuchukuliwa haraka
Awali Meneja wa mgodi wa MMG, Esther Kijonga (wa pili kulia) akitoa ufafanuzi kwa Naibu Waziri wa Madini Mhe. Doto Mashaka Biteko (wa pili kushoto) alipokuwa akikagua mgodi huo.
Tazama hapa chini BMG Online Tv

No comments:

Powered by Blogger.