Sijawahi baguliwa wala kunyanyaswa- Diwani Chadema
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Diwani wa
Kata ya Uyovu wilaya ya Bukombe mkoani Geita, Mhe.Yusuph Fungameza (Chadema)
amesema tangu achaguliwe kuwatumikia wananchi kupitia nafasi hiyo, hawajawi
kubaguliwa kwenye vikao vya halmashauri kutokana na asilimia kubwa ya madiwani
kuwa wa CCM.
Mhe.Fungameza
ameyasema hayo wakati akitoa salamu zake kwenye mkutano wa hadhara wa mbunge wa
jimbo la Bukombe, Mhe.Doto Biteko (CCM) ambaye pia ni Naibu Waziri wa Madini,
uliofanyika katika Kijiji cha Kabulima, Uyovu.
Kwenye
mkutano huo, takribani wanachama 10 wa Chadema walijiunga na CCM.
No comments: