ALAT Mwanza yachangia miradi ya elimu, yaitunuku Magu cheti cha pongezi
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
SOMA Rais Magufuli atunukiwa cheti cha pongezi
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Jumuiya ya
Serikali za Mitaa Tanzania (ALAT) tawi la Mkoa wa Mwanza imetoa shilingili
Milioni 3.8 kwa ajili ya kuchangia ukamilishaji wa miradi ya elimu katika
Halmashauri za Wilaya Kwimba na Sengerema.
Akikabidhi
fedha hizo kwa Wakurugenzi wa Halmashauri hizo, Mwenyekiti wa ALAT mkoani
Mwanza, Hilali Elisha amesema shilingi Milioni mbili ni kwa ajili ya kuchangia ujenzi
wa bweni la wanafunzi wa kike katika shule ya Msingi Nyamatongo Wilaya Sengerema
na shilingi Milioni 1.8 kuchangia ujenzi wa shule ya Msingi Kakola wilayani
Kwimba.
Pia jumuiya
hiyo imekabidhi cheti cha pongezi kwa Halamshauri ya Wilaya Magu kwa kuongoza
katika ukusanyaji wa mapato kwa mwaka wa fedha 2017/18 ambapo ilikusanya
asilimia 106 ikifuatiwa na Halmashauri za Misungwi 80, Ukerewe 80, Jiji la
Mwanza 74, Kwimba 74, Sengerema 70, Buchosa 60 na Ilemela 42.
Hayo
yalijiri jana kwenye kikao cha ALAT mkoani Mwanza kilichofanyika jana wilayani
Magu.
Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya Magu, Lutengano Mwalwiba (kulia) akipokea cheti cha pongezi baada ya Halmashauri hiyo kuongoza katika ukusanyaji wa mapato miongoni mwa Halmashauri za Mkoa Mwanza
Mkurugenzi Halmashauri ya Kwimba, Upendo Malabeja (kushoto) akipokea hundi ya shilingi Milioni 1.8 kwa ajili ya kuchangia
ujenzi wa shule ya Msingi Kakola
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Sengerema, Magesa Mafuru (kushoto) akipokea hundi ya shilingi Milioni mbili kwa ajili ya kuchangia ujenzi bweni la wanafunzi wa kike katika shule ya msingi Nyamatongo
Mwenyekiti wa ALAT mkoani Mwanza, Hilali Elisha akizungumza kwenye mkutano huo
Tazama BMG Online Tv hapa chini
SOMA Rais Magufuli atunukiwa cheti cha pongezi
No comments: