Rais Magufuli atunukiwa cheti cha pongezi
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza hivi karibuni alipofanya ziara ya kikazi mkoani Mwanza.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Jumuiya ya
Serikali za Mitaa Tanzania (ALAT) tawi la Mkoa wa Mwanza imemtunuku Mhe. Rais
Dkt. John Pombe Magufuli cheti cha pongezi.
Cheti hicho
kimepokelewa jana na Mkuu wa Mkoa Mwanza Mhe. John Mongella aliyewakilishwa na
Mkuu wa Wilaya Sengerema Mhe. Mwl. Emmanuel Kipoke kwenye mkutano wa ALAT uliofanyika
wilayani Magu.
Baada ya
kukabidhi cheti hicho, Mwenyekiti wa ALAT mkoani Mwanza, Hilali Elisha ambaye
pia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Magu akazungumza na BMG Online Tv na
kueleza sababu za jumuiya hiyo kumtunuku Mhe. Rais Dkt. Magufuli cheti cha
pongezi.
Mwenyekiti wa ALAT mkoani Mwanza, Hilali Elisha (kushoto) akimkabidhi Mkuu wa Wilaya Sengerema Mhe. Mwl. Emmanuel Kipole (kulia) aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa Mwanza cheti cha kumpongeza Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli
Tazama BMG Online Tv hapa chini
SOMA Malengo ya wana Bujora kupata shule ya sekondari yatimia
No comments: