DC Misungwi apiga marufuku usafirishaji wa madini ghafi
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
SOMA Washindi UMITASHUMTA 2018 wilayani Misungwi wapongezwa
Mkuu wa wilaya Misungwi, Mhe. Juma Sweda akizungumza kwenye kikao cha baraza la madiwani.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Mkuu wa wilaya
Misungwi mkoani Mwanza Juma Sweda amepiga marufuku usafirishaji wa madini ghafi
(Cabon) kutoka ndani ya wilaya hiyo kwa ajili ya kwenda kuchenjuliwa katika
wilaya nyingine.
Sweda alitoa
zuio hilo jana wakati akizungumza kwenye mkutano wa baraza la madiwani wa halmashauri
ya wilaya Misungwi, na kuwataka madiwani na watendaji kusimamia kikamilifu
utekelezaji wake.
Alisema
lengo la kuzuia usafirishaji wa madini ghafi hayo ikiwemo dhahabu na chuma ni
kuhakikisha uchenjuaji unafanyikia ndani ya wilaya ya Misungwi ili kuongeza
fursa ya ajira kwa wananchi pamoja na ukusanyaji mapato hivyo madini hayo
yatasafirishwa baada ya kuongezwa thamani katika eneo (halmashauri) yanapochimbwa
kama sheria ya madini inavyoelekeza.
Naye
Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya Misungwi, Antony Bahebe alisisitiza
madiwani na watendaji wa halmashauri hiyo kuhakikisha wanasimamia vyema suala
la ukusanyaji wa mapato ili kufikia lengo la asilimia 100 mwaka 2018/19 kutoka
asilimia 80.16 mwaka 2017/18 huku wakihakikisha hakuna upotevu wa mapato ya
halmashauri hiyo na kwamba watakaoshindwa kufanya hivyo hatua za kinidhamu
zitachukuliwa dhidi yao.
Kwa upande
wake Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo, Kisena Mabuba alisema zuio hilo
litasaidia kudhibiti mapato yanayopatikana kutokana na shughuli za uchenjuaji
madini hivyo atashirikiana vyema na watendaji wake ili kutekeleza vyema zuio
hilo.
Pamoja na
kujadili taarifa ya maendeleo ya halmashauri ya Misungwi kwa kipindi cha robo
ya nne ya mwaka 2017/18, pia baraza hilo lilifanya uchaguzi wa Makamu
Mwenyekiti ambapo diwani wa Kata ya Fella, Paul Kishinda alichaguliwa bila kupingwa
kwa kura 34 kushika nafasi hiyo iliyokuwa ikishikiliwa na diwani wa Kata ya
Mabuki, Nicodem Ihano.
Mhe. Juma Sweda akizungumza kwenye kikao cha baraza la madiwani halmashauri ya Misungwi
Mwenyekiti halmashauri ya Misungwi, Antony Bahebe akizungumza kwenye kikao hicho
Mkurugenzi halmashauri ya Misungwi, Mwl. Kisena Mabuba akizungumza kwenye kikao hicho
Makamu Mwenyekiti halmashauri ya Misungwi, Katikista Paul Kishinda (CCM) ambaye alichaguliwa jana akitoa salamu za shukurani kwa kuchaguliwa kwa kishindo
Makamu Mwenyekiti mstaafu halmashauri ya Misungwi, Nicodem Ihano akitoa salamu za shukurani baada ya kustaafu
Zoezi la kuhesabu kura kumpata Makamu Mwenyekiti halmashauri ya Misungwi kwa mwaka 2018/19
Tazama BMG Online Tv hapa chini
SOMA Washindi UMITASHUMTA 2018 wilayani Misungwi wapongezwa
No comments: