Washindi UMITASHUMTA 2018 wilayani Misungwi wapongezwa
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
SOMA Halmashauri ya Misungwi yaibuka bingwa mashindano ya UMITASHUMTA
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Baraza la
madiwani katika Halmashauri ya wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza limewapongeza wachezaji
walioshiriki mashindano ya umoja wa michezo, sanaa na taaluma kwa shule za
msingi UMITASHUMTA 2018 baada ya kuibuka na ushindi.
Mwenyekiti
wa Baraza hilo, Antony Bahebe ametoa pongezi hizo leo kwenye mkutano wa robo ya
nne ya mwaka 2017/18, uliolenga kujadili taarifa za maendeleo za mwaka.
Kupitia
kikao hicho, Baraza hilo limepokea rasmi makombe 14 ya ushindi yaliyotokana na
ushindi huo na kuahidi kuandaa zawadi maalum kwa ajili ya wachezaji hao ambapo itakabidhiwa
hivi karibuni.
Afisa
Michezo Wilaya Misungwi, Mwl. Sixbert Mbwambo amesema katika mashindano hayo
yaliyofanyika Mei 31 hadi June 03 mwaka huu katika kituo cha shule ya sekondari
ya wavulana Bwiru, wilaya hiyo iliibuka mshindi wa kwanza kwa mkoa Mwanza na
kujinyakulia vikombe 14 kati ya 21.
Mwl. Mbwambo
amesema wilaya Misungwi ilitoa wanafunzi 34 kati ya 120 ili kutengeneza timu ya
mkoa Mwanza iliyoshiriki mashindano ya UMITASHUMTA kitaifa ambapo Mwanza
iliibuka mshindi wa kwanza.
Wachezaji
waliopongezwa wanaunda wa timu za michezo ya aina mbalimbali ikiwemo mpira wa
miguu, pete,mikono, wavu na riadha ambapo wametoa pongezi kwa baraza hilo na
kuahidi kufanya vizuri zaidi katika mashindano yajayo.
Pia
itakumbukwa kwamba Halmashauri ya Misungwi iliibuka nafasi ya nne kati ya
Halmashauri nane mkoani Mwanza kwenye mashindano ya umoja wa michezo, sanaa na
taaluma kwa shule za sekondari UMISSETA 2018 yaliyofanyika kituo cha shule ya
sekondari Nsumba huku mkoa Mwanza ukiibuka nafasi ya pili kitaifa.
Mwenyekiti Halmashauri ya Mwisungwi, Antony Bahebe (kushoto), pamoja na Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri hiyo Mwl. Kisena Mabuba (kulia) wakiwa na kombe la ushindi mashindano ya UMITASHUMTA ngazi ya mkoa Mwanza
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM wilayani Misungwi, Daud Gambadu (kushoto), pamoja na Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe. Juma Sweda (kulia) wakiwa na kombe la ushindi mashindano ya UMITASHUMTA ngazi ya mkoa Mwanza
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM wilayani Misungwi, Daud Gambadu (kulia), pamoja na Katibu wa CCM wilayani Misungwi Latifa Malimi (kushoto) wakiwa na kombe la ushindi mashindano ya UMITASHUMTA ngazi ya mkoa Mwanza
Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya wilaya Misungwi, Mwl Kisena Mabuba akizungumza kwenye mkutano wa Baraza la Madiwani wa Halmashauri hiyo
Afisa Elimu Msingi wilayani Misungwi, Mwl. Ephraim Majinge akifurahia ushindi wa wanafunzi wake
Wachezaji wa UMITASHUMTA 2018 wakiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi mbalimbali
Tazama BMG Online Tv hapa chini
SOMA Halmashauri ya Misungwi yaibuka bingwa mashindano ya UMITASHUMTA
No comments: