MWANZA: Ibungilo waibuka mabingwa Angeline Jimbo Cup 2018
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
Judith Ferdinand, BMG
Timu ya Kata
ya Ibungilo imeibuka mabingwa wa mashindano ya Angeline Jimbo Cup msimu wa
2018/19 baada ya kuilaza Kirumba kwa goli 4-1.
Katika
mchezo wa fainali uliotimua vumbi leo kwenye uwanja wa CCM Kirumba, Ibungilo
ilifunga goli dakika ya nane kupitia mshambuliaji wake Yusuph Amran huku Kirumba ikisawazisha dakika ya 77 na hivyo hadi
dakika 90 matokeo yalikuwa 1-1.
Baada ya
dakika 90 za mchezo huo, ilifuata mikwaju ya penalt ambapo Ibungilo ilipata mikwaju
mine huku Kirumba ikifunga mkwaju mmoja na kukosa mikwaju miwili na hivyo kuibuka
mabingwa wa msimu huu.
Akizungumza baada
ya kumalizika kwa mchezo huo, kocha wa Ibungilo Swala Daud alisema anamshukuru
Mungu kuibuka na ushindi huo pamoja na mashabiki waliojitokeza kuwaunga mkono
pamoja na mbunge wa Jimbo la Ilemela
Dkt.Angeline Mabula kwa kuandaa mashindano hayo ambayo yamesaidia vijana
kuonyesha vipaji na kuibua vipya ambapo msimu wa 2016 ilishika nafasi ya pili
na wanajipanga na msimu ujao.
Naye Kocha
wa timu ya Kirumba, Iddi Kilewa alisema wamepoteza mchezo huo baada ya
kushindwa kutumia nafasi walizozipata hivyo wanajipanga na msimu ujao huku
akimuomba Dkt.Mabula msimu ujao waachie Chama cha Soka Mkoa wa Mwanza(MZFA)
ndio wachezeshe na kusimamia ili kuleta usawa na sheria 17 za mpira zifuatwe.
Kwa upande
Dkt.Mabula alisema mashindano hayo yamelenga kuendeleza na kuibua vipaji vipya
vinavyopatikana kwenye jimbo lake huku akisisitiza kuwa yatafanyika kila mwaka
mara baada ya kupatikana shiriki sanjari na
kuwaomba viongozi na wananchi wa jimbo hilo kuunga mkono jitihada
anazozichukua katika kuhakikisha wilaya ya Ilemela inaendelea kuwa kitovu
cha kuzalisha vipaji vya michezo
mbalimbali nchini.
Naibu Waziri Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na
Walemavu Athony Mavunde ambaye alikuwa mgeni rasmi katika fainali hiyo
alimpongeza Dkt.Mabula kwa kuaandaa mashindano hayo kwa ajili ya kuendeleza
michezo kwa vijana kama ilivyo dhima ya serikali hivyi aliwaomba wabunge na
viongozi wengine kuiga mfano.
Timu ya Ibungilo
imejinyakulia kitita cha Milioni mbili, kombe, mpira mmoja pamoja na seti moja
ya jezi, mshindi wa pili timu ya Kirumba
imepata Milioni 1.5, kombe, jezi seti
moja na mpira mmoja huku mshindi wa tatu timu ya Shibula ikiibuka na Milioni 1,
kombe, mpira pamoja na jezi seti moja.
No comments: