Profesa Kikula aongoza kikao kazi Tume ya Madini
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
Mwenyekiti
wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula.
Na Greyson
Mwase, Tume ya Madini
Jna Septemba
25, 2018 Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula aliongoza kikao kazi
cha tume hiyo Jijini Dodoma kilicholenga kujadili utendaji kazi wake katika kipindi
cha robo mwaka (Julai hadi Septemba).
Kikao hicho
kilishirikisha pia viongozi mbalimbali wakiwemo Katibu Mtendaji wa Tume ya
Madini Profesa Shukrani Manya, Makamishna wa Tume Dkt. Athanas Macheyeki,
Profesa Abdulkarim Mruma, Haroun Kinega,
Dkt. Florens Tunuka, Dkt. Evaristo Longopa pamoja na watendaji wengine kutoka
Tume.
Kati ya
masuala yaliyojadiliwa katika kikao hicho ni pamoja na kupata taarifa za
utendaji za kamati za Tume ya Madini katika kipindi cha robo mwaka na namna ya
uboreshaji wa huduma za leseni.
No comments: