Ukweli kuhusu fedha za ujenzi wa meli mpya Ziwa Victoria
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
Serikali ya
Tanzania kupitia kampuni ya Huduma za Meli (MSCL) imeingiamikataba mine ambayo
ni ujenzi wa meli mpya nay a kisasa katika Ziwa Victoria, chelezo na ukarabati
wa meli za Mv. Victoria na Mv. Butiama na kampuni kutoka Jamhuri ya Korea
Kusini wenye thamani ya shilingi bilioni 152.
Meli hiyo
mpya ya abiria na mizigo itakuwa na uwezo wa kubeba abiria 1,200, tani 400 za
mizigo na magari madogo 20 ambapo mkandarasi ni M/S Gas Entec Company Limited ya
Korea Kusini akishirikiana na SUMA JKT kutoka Tanzania na kampuni ya KANGNAM
Corporstion ya Korea Kusini pia kwa gharama ya shilingi bilioni 88.764 na
unatarajiwa kukamilika kwa muda wa miaka miwili.
Aidha ujenzi
wa chelezo itakayotumika kwa ajili ya ujenzi wa meli mpya utatekelezwa na
mkandarasi M/S STX Engine Company Limited akishirikiana na kampuni ya SAEKYUNG
Construction Company Limited zote kutoka Korea Kusini kwa gharama ya shilingi
bilioni 35.994 na ujenzi huo utachukua muda wa mwaka mmoja.
Pia
ukarabati wa meli za Mv. Victoria na Mv. Butiama utatekelezwa na kampuni ya
KTMI Co.LTD ya Korea Kusini ikishirikiana na kampuni ya YUKO’S Enterprises (EA)
Co.Ltd kwa gharama za shilingi bilioni 27,009,738,200 ambapo shilingi bilioni
22,712,098,200 ni kwa ajili ya ukarabati wa meli ya Mv. Victoria na shilingi
bilioni 4,897,640,000 ni kwa ajili ya ukarabati wa meli ya Mv. Butiama.
Akizungumza
baada ya kushuhudia zoezi la utilianaji saini mikataba hiyo, Mhe. Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli alielezea chanzo cha fedha
hizo.
Balozi wa Korea Kusini hapa nchini Song Geum Yong akizungumza kwenye hafla hiyo
Mikataba iliyosainiwa leo
Tazama hapa chini BMG Online Tv
No comments: