Biteko awaonya wasio na vifaa kinga machimbo ya jasi wilayani Same
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
Naibu Waziri
wa Madini Mwl. Doto Mashaka Biteko (kulia) akizungumza na baadhi ya wachimbaji wa
madini ya viwandani aina ya jasi (Gypsum) ya Chakoko yaliyopo katika Kijiji cha Makanya wilaya ya
Same mkoani Kilimanjaro.
Mwl. Biteko
alifanya ziara ya kutembelea machimbo hayo na baadae kuzungumza na wachimbaji na
wamiliki wa leseni za madini ambapo aliwataka wamiliki wote wa leseni katika
machimbo hayo kuhakikisha wanazingatia usalama mahala pa kazi kwa kuwapa
wafanyakazi vifaa kinga ikiwemo kofia ngumu pamoja na vikinga vumbi.
Alimwagiza
Afisa Madini mkoani Kilimanjaro, Fatma Kyando kuhakikisha agizo hilo
linatekelezwa ndani ya wiki tatu na kwamba watakaoshindwa kufanya hivyo hatua
kali za kisheria zichukuliwe dhidi yao.
Mmoja wa wachimbaji madini ya jasi aliyekutwa hana vifaa kinga katika machimbo ya Chakoko wilayani Same.
Tazama BMG Online Tv hapa chini
SOMA>>>Wamiliki wa leseni Mererani watakiwa kulipa madeni yao
No comments: