Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo akabidhiwa rasmi Tume ya Taifa ya Umwagiliaji
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
Katibu Mkuu wa wizara ya kilimo Mhandisi Mathew Mtigumwe (Kulia) akizungumza jambo wakati wa mkutano wa waandishi wa habari uliofanyika katika Ukumbi wa Wizara ya Maji Mjini Dodoma wakati wa makabidhiano ya nyaraka muhimu kuhusu Tume ya Umwagiliaji. Kushoto ni Katibu Mkuu wa wizara ya maji Prof Kitila Mkumbo.
Mkutano wa waandishi wa habari ukiendelea katika Ukumbi wa
Wizara ya Maji Mjini Dodoma wakati wa makabidhiano ya nyaraka muhimu kuhusu
Tume ya Umwagiliaji.
Katibu Mkuu wa wizara ya Maji Prof Kitila Mkumbo (Kushoto)
akizungumza jambo wakati wa mkutano wa waandishi wa habari uliofanyika katika
Ukumbi wa Wizara ya Maji Mjini Dodoma wakati wa makabidhiano ya nyaraka muhimu
kuhusu Tume ya Umwagiliaji. Kulia ni Katibu Mkuu wa wizara ya kilimo Mhandisi
Mathew Mtigumwe.
Na Mathias Canal, WK-Dodoma
Katika
kuongeza ufanisi kwenye matumizi ya umwagiliaji katika kilimo kama sehemu ya
utekelezaji wa Programu ya kuendeleza sekta ya kilimo awamu ya pili
(Agricultural Sector Development Programme -Phase Two -ASDP II) rasmi Katibu
Mkuu wa Wizara ya kilimo Mhandisi Mathew Mtigumwe amekabidhiwa Tume ya
Umwagiliaji na katibu Mkuu wa wizara ya maji Prof Kitila Mkumbo.
Uamuzi huo
wa Tume ya umwagiliaji kuhamishiwa wizara ya kilimo unalenga kuiwezesha wizara
yenye dhamana ya sekta ya maji kudhibiti matumizi ya maji katika umwagiliaji
bila kuwa na mgongano wa kimajukumu.
Imeelezwa
kuwa sekta ya umwagiliaji ndiyo inayoongoza kwa matumizi ya maji hapa
nchini ambapo kwa sasa kiwango cha
matumizi ya maji kwa ajili ya umwagiliaji kinakadiriwa kuwa mita za ujazo
milioni 10,309 kwa mwaka ambacho ni sawa na asilimia 83.6 ya matumizi ya maji
yote hapa nchini.
Kufuatia
uamuzi huu wa serikali Tume ya umwagiliaji sasa itawajibika kiutawala kwa
katibu Mkuu wa wizara ya kilimo na hivyo jina la wizara ya maji kubadilika na
kuwa wizara ya Maji.
Katika
kutekeleza maamuzi ya serikali ya kuhamishia wizara ya kilimo jukumu la
umwagiliaji, leo tarehe 10 Octoba 2018 Katibu Mkuu wa wizara ya kilimo Mhandisi
Mathew Mtigumwe na Katibu Mkuu wa wizara ya maji Prof Kitila Mkumbo wamefanya
makabidhiano ya nyaraka muhimu kuhusu Tume ya Umwagiliaji zikiwemo sera ya
umwagiliaji, Sheria ya umwagiliaji, na mpango kabambe wa Umwagiliaji (Revised
National Irrigation Master Plan).
Utekelezaji
wa maamuzi ya serikali kuhamishia jukumu la umwagiliaji kwenda wizara ya kilimo
utaendelea kutekelezwa hatua kwa hatua katika mwaka wote huu wa fedha 2018/2019
na utakamilika kwa marekebisho ya Hati ya mgawanyo wa majukumu ya wizara ya
Maji na Wizara ya kilimo.
No comments: