Maonesho ya SIDO 2018 kitaifa mkoani Simiyu
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Matangazo.
Waziri wa
kilimo Mhandisi Dkt Charles Tizeba (Mb)
akisisitiza jambo wakati akizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe Antony Mtaka
pamoja na kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa Mara baada ya kuwasili Mkoani Simiyu
kwa ziara ya kikazi ya siku moja, leo Alhamisi Octoba 2018.
Waziri wa kilimo Mhandisi Dkt Charles Tizeba (Mb) akiwa ameambatana na mwenyeji wake Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe Antony Mtaka kutembelea mabanda mbalimbali ya Maonesho ya Kitaifa ya Viwanda Vidogo (SIDO), yanayofanyika katika Viwanja vya Nyakabindi katika Halmashauri ya mji wa Bariadi mkoani Simiyu.
Waziri wa kilimo Mhandisi Dkt Charles Tizeba (Mb) akizungumza jambo mara baada ya kuwasili kutembelea mabanda mbalimbali ya Maonesho ya Kitaifa ya Viwanda Vidogo (SIDO), yanayofanyika katika Viwanja vya Nyakabindi katika Halmashauri ya mji wa Bariadi mkoani Simiyu.
Waziri wa kilimo Mhandisi Dkt Charles Tizeba (Mb) akizungumza jambo wakati akikagua mashine zinazotengenezwa na SIDO TDC kwa ajili ya uchakataji wa mazao mara baada ya kutembelea mabanda mbalimbali ya Maonesho ya Kitaifa ya Viwanda Vidogo (SIDO), yanayofanyika katika Viwanja vya Nyakabindi katika Halmashauri ya mji wa Bariadi mkoani Simiyu.
Na mathias Canal-WK, Bariadi-Simiyu
Waziri wa
kilimo Mhandisi Dkt Charles Tizeba (Mb)
leo Alhamisi Octoba 2018 amewataka wajasiriamali kote nchini kuchangamkia fursa
ya kutembelea katika Maonesho ya Kitaifa ya Viwanda Vidogo (SIDO),
yanayofanyika katika Viwanja vya Nyakabindi katika Halmashauri ya mji wa
Bariadi mkoani Simiyu.
Katika
maonesho hayo ambayo yalianza Oktoba 23 mwaka huu, Dkt Tizeba amesema kuwa hiyo
ni fursa kwa wananchi kuweza kujielimisha katika maeneo mbalimbali ya
teknolojia za viwanda hususani viwanda vidogo, lakini pia wajasiriamali kupata
nafasi ya kujifunza kutoka kwa wenzao wa maeneo mengine nchini na nje ya nchi.
"Nitoe
wito kwa wananchi wa mkoa wa Simiyu na mikoa ya jirani kama Mara, Mwanza na
Shinyanga wajitokeza kwa wingi kushiriki
maonesho haya maana hii ni fursa muhimu kwao katika kuakisi kwa vitendo
Tanzania ya viwanda" Alisema Dkt Tizeba.
Dkt Tizeba
amempongeza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe Antony Mtaka kwa kubuni jambo hilo
sambamba na kumpongeza Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe Charles
Mwijage kwa kuwaalika wajasiriamali, na wataalamu waoneshaji wa teknolojia
mbalimbali kwani jambo hilo litatoa fursa kwa wananchi wa Mkoa wa Simiyu na
mikoa mingine kuona ushindani katika uongezaji wa thamani wa mazao mbalimbali
na fursa kwa wajasiriamali kujifunza kutoka kwa wenzao.
Aidha, Dkt
Tizeba amesema kuwa Maonesho hayo ya SIDO ambayo ni ya kwanza kufanyika Kitaifa
yatawasaidia wajasiriamali kote nchini kupanua masoko ya bidhaa zao.
Maonesho ya
Kitaifa ya Viwanda Vidogo (SIDO) yakiwa na Kauli Mbiu isemayo PAMOJA TUJENGE
VIWANDA KUFIKIA UCHUMI WA KATI”. yalifunguliwa rasmi na Waziro Mkuu wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania Mhe Kassim Majaliwa (Mb) siku ya Jumanne Oktoba 23,
2018 na yanatarajiwa kuhitimishwa siku ya Jumapili Oktoba 28, 2018.
No comments: