Biteko awataka wawekezaji kuandaa mipango ya kuhudumia wanajamii
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
Mwandishi Maalum
Naibu Waziri
wa Madini, Doto Biteko amewataka wawekezaji katika sekta ya madini kuandaa mipango
kazi ya namna ya kutoa huduma za maendeleo katika jamii na kuiwasilisha kwa
wakurugenzi wa halmashauri husika ili kushirikiana katika kutekeleza mipango
hiyo.
Biteko
alitoa agizo hilo jana alipofanya ziara ya kikazi ya kukagua shughuli za
uchimbaji madini katika Kijiji cha Maseyu mkoani Morogoro.
Aidha Biteko
alikemea tabia za baadhi ya viongozi wa serikali kuomba kwa wawekezaji kwa
ajili ya kuendeshea vikao na badala yake wawe na mipango ya kimaendeleo.
Alisema
wawekezaji katika eneo husika wanapaswa kusaidia katika utekelezaji wa miradi
ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa zahanati, shule na barabara miradi ambayo
itakuwa ikikumbukwa hata baada ya madini kuisha katika maeneo hayo.
Aliwaasa wananchi
na viongozi kutumia kodi zinazotokana na uwekezaji huo katika kutekeleza miradi
yenye tija na kueleza kuwa madini yana mwisho hivyo ni vyema kuhakikisha kuna
miradi endelevu itakayosalia kama kumbukumbu.
No comments: