Mfuko wa NHIF watoa onyo kwa wanaoazimana kadi za matibabu
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
Judith Ferdinand, BMG
Wanachama wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) wameonywa kuacha
kufanya udanganyifu wa matumizi ya kadi
moja kwa zaidi ya mtu mmoja kwani ni kinyume cha sheria.
Onyo hilo
limetolewa na Meneja wa mfuko huo mkoani Mwanza, Jarlath Mushashu wakati
akizungumza kwenye kikao cha washauri na viongonzi wa wanafunzi kilichofanyika jana
jijini Mwanza.
Alisema kumekuwa na tabia kwa baadhi ya
wanachuo pamoja na wananchi ambao ni wanachama wa mfuko huo kwa mhusika kumpatia
mtu mwingine kadi ya bima ili akapatiwe matibabu.
"Kitendo
cha mwanachama kumpatia kadi mtu mwingine ili apatiwe matibabu ni kinyume cha
sheria kwani ni kuhujumu mfuko na kuwakosesha ambao ni wanachama kupata fursa
ya matibabu hivyo wenye tabia hiyo waache na atakayebainika sheria itafuata
mkondo wake". Alisema Mushashu.
Mushashu alitumia
fursa hiyo kuwahimiza wanachuo na wananchi kwa ujumla kujiunga na bima ya afya
ambayo humsaidia mwanachama kuwa na uhakika wa matibabu wakati wote bila
kujali hali ya kifedha na kiafya
aliyonayo kwa wakati huo.
Pia alisema kupitia
bima, mwanafunzi anapata matibabu ambayo ni gharama pale anapougua hata akiwa
nje ya chuo ama mkoa mwingine katika kipindi cha likizo na bila kujali hali ya
kiafya aliyonayo mwanachama.
Naye Afisa Matekelezo kutoka NHIF Mkoa Mwanza,
Ricky Jonathan alisema changamoto
iliyopo ni wanachuo kutokuwa na elimu ya uelewa kuhusu masuala ya mbima hatua
inayosababisha kuazimishana kadi, kutokuwa na kiupaumbele cha bima ya afya kama
ajenda ya kudumu.
Baadhi ya
wanafunzi waliohudhuria kikao hicho walitoa shukurani kwa mfuko wa NHIF na
kuahidi kutumia vyema elimu waliyoipata ili kunufaika na huduma ya matibabu inazotolewa
kupitia mfuko huo.
No comments: