LIVE STREAM ADS

Header Ads

Umoja wa Makondakta Mwanza wagawa sare kwa wanachama wake

Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.

 Judith  Ferdinand, BMG
Katika kuhakikisha wanaondoa vitendo vya kihalifu ikiwemo utumiaji wa dawa za kulevya, lugha za matusi na wizi katika maeneo ya stendi, makondakta na wasaidizi wao (wapiga debe) wa daladala mkoani Mwanza wameanzisha umoja wao.

Akizungumza katika kikao maalumu kwa ajili ya kuwagawia sare wanachama wa umoja huo, Mwenyekiti wa umoja wa Makondakta na wasaidizi wao (UVDS) Mkoa wa Mwanza, Mrimi Juma alisema lengo la kuanzisha umoja huo ni kutatua kero zinazotokea katika maeneo ya stendi pamoja na kubadili mtazamo wa abiria na jamii ambayo imekuwa ikiwachukulia kama walevi, wezi na kuwa ni vijana wasio jitambua sanjari na kusaidizana katika masuala mbalimbali.

Juma alisema kupitia umoja huo ambao mpaka sasa unajumla ya wanachama 500, watakuwa na sare ambazo zina namba pembeni, zitakazosaidia kuwatambua kama ni wanachama na endapo watafanya uhalifu itakuwa ni rahisi kuwagundua kwani kupitia namba hizo tutamjua muhusika kwani kuna baadhi wanafanya uhalifu alfu wanasingiziwa wapiga debe.

Aliahidi kuwa Disemba mwaka huu kila wanachama atakatiwa  bima ya afya ambayo itawasaidia katika kupata matibabu ambayo yanagharama kubwa licha ya kuchangishana fedha pale mwenzao anapokuwa amepata matatizo ila hazitoshi ukilinganisha na kipato chao,na kuanzia januari hadi februari mwakani watawapeleka  chuo cha Veta ili waweze kupata leseni.

Kwa upande wake Polisi Kata wa Kata ya Buhongwa, Afande Juma Salum ambaye alikuwa mgeni rasmi katika  kikao hicho aliwataka makondakta na wasaidizi wao kuipenda kazi yao kwa kuwa wasafi na kuacha lugha za matusi kwani kazi hiyo ni kama nyingine na wahakikishe wanafuata na kutekeleza yale waliokubaliana yeye atayasimami na kwenye kazi hana urafiki na mtu anacho angalia ni sheria.

Suala la sare kwa wanachama wa umoja huo ni zuri kwani litawasaidia kujua nani siyo mwenzao, pia wawe na utaratibu wa kuhakikisha kila asubuhi wanaripoti na kusaini kwa viongozi wa umoja huo katika vituo vyao vya kufanyia kazi, kwani jicho la wengi lilikua likiwaangalia tofauti na kuwaona ni wahuni.


Naye Katibu wa umoja huo, Erick Felician alisema lengo la umoja huo ni kusaidiana katika shida na raha ikiwemo kukopeshana mikopo ambayo haina riba ili waweze kukikomboa kiuchumi kwa kuanzisha shughuli za ujasiriamali pamoja na kuanzisha timu inayotokana na umoja huo kwani wanaamini michezo ni ajira na huleta watu pamoja.
Mwenyekiti wa Umoja wa Makondakta mkoani Mwanza (UVDS), Mrimi Juma akizungumza katika kikao na wanachama wake kilichofanyika jumapili iliyopita katika ofisi za umoja huo Buhongwa Jijini Mwanza.

No comments:

Powered by Blogger.