Wajasiriamali Mwanza watakiwa kutumia vyema fursa zinazowazunguka
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
Judith Ferdinand, BMG
Wajasiriamali wamehimizwa kutumia vyema fursa zinazojitokeza
ikiwemo mradi wa kuwasaidia na kuwaendeleza wajasiriamali Tanzania(TLED) pamoja
na kuweka mazingira bora katika kuendeleza biashara zao.
Wito huo
umetolewa na Afisa Biashara Mkoa wa
Mwanza, Anthony Yessaya wakati akizungumza katika sherehe ya maadhimisho ya miaka 60
nchini ya shirika la Voluntary Service Overseas (VSO) linalosimamia mradi wa TLED, yaliyofanyika Jijini Mwanza na kukutanisha wanufaika wa mradi huo kutoka Mwanza na Shinyanga.
Alisema hata kama mradi utaisha
wajasiriamali hao wanatakiwa kuwa na kitu cha kujivunia ambacho kitakuwa
kumbukumbu katika maendeleo ya biashara zao hivyo watumie fursa hiyo na
nyingine zinazopatikana vizuri.
Yessaya
alieleza kwamba katika mkoa wa Mwanza, mradi wa TLED
umekuwa na manufaa kwa wajasiriamali kwani wameweza kukutanishwa na taasisi za
kifedha ambazo zinawasaidia kuwapa mkopo kwa ajili ya kuendeleza biashara zao,
elimu ya utunzaji fedha na kumbukumbu, soko pamoja na kuwakutanisha na mamlaka
za udhibiti ubora wa bidhaa kama TFDA na TBS.
Alisema ili mradi utoke kwa shirika na kwenda wa
wananchi ambao ndio walengwa uongozi wa VSO unatakiwa kushirikisha wadau mbalimbali
ili wachangie mawazo yao ambayo
yatasaidia katika kuboresha na kufikia malengo pale wanapofanya tathimini ya
mradi.
Pia alisema mradi unamanufaa makubwa kwa wajasiriamali hivyo ni fursa ya viongozi wa Chemba
ya Wafanyabiashara,Wenye Viwanda na Kilimo Tanzania (TCCIA) na Chemba ya
Wanawake Wafanyabiashara Tanzania (TWCC)
kuwahimiza wanachama wao.
Justas
alisema katika kuwasaidia wajasiriamali kwa kushirikiana na Chemba ya Wafanyabiashara Wenye Viwanda na Kilimo
Tanzania(TCCIA), Chemba ya Wanawake Wafanyabiashara Tanzania (TWCC) Shirika la
Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO) wamekua wakifanya kazi kwa ukaribu, ambapo
kupitia SIDO wajasiriamali wanaweza kupata kibali cha biashara kutoka TBS na
TFDA ili kupata bidhaa zenye viwango na kuwekeza kwenye viwanda kama serikali inavyotaka.
"Mradi
unatoa mafunzo kwa wajasiriamali wadogo kuhusu
biashara, kuuza, usimamizi wa fedha pamoja na teknolojia, huku lengo
likiwa ni kuboresha ujuzi kuhusu fursa katika masuala ya masoko, jinsi ya
kufanya bishara na elimu ya ufundi sambamba na kuongeza uelewa wa wanawake
kwenye kuanzisha na kukuza biashara ndogo ambazo ni endelevu," alisema
Justas.
Pia alisema,
waliweza kuwaleta wajasiriamali 20, 10 wakitokea Mwanza na wengine Shinyanga
katika maonesho ya biashara Afrika Mashariki yaliyofanyika septemba ikiwa ni fursa
ya kupata masoko, hivyo faida ilionekana baada ya Waziri wa Viwanda, Biashara na
Uwekezaji Dkt.Charles Mwijage alipotembelea banda lao aliiagiza TBS kusajili bidhaa
za wajasiriamali wawili ambao wako chini ya TLED.
Hata hivyo
alisema katika mradi huo, wana Mfuko wa Ufumbuzi wa Teknolojia (Technological Innovation
Fund) ambao ni kwa ajili ya kuwawezesha
wajasiriamali mashine kwa ajili ya shughuli za uzalishaji bidhaa kwa wingi na
bora kama lilivyo lengo la Serikali la kuwa na viwanda.
Awamu ya kwanza
wamewapatia mashine jumla wajasiriamali 13 mbao sita kutoka mkoani Mwanza
huku saba wakiwa wa Shinyanga, kwa
sasa watu wamejaza fomu kwa ajili ya maombi ya awamu ya pili na wanatarajia wataongezeka.
Kwa upande
wake Meneja Mradi wa Kuwawezesha Vijana
Kanda ya Ziwa wa VSO, Haidari Mfinanga alisema shirika hilo limekuwa
likishughulika katika miradi ya kijamii nchini kama elimu, afya huku mikoa ya
Mwanza na Shinyanga limejikita katika
mradi wa kujikimu wa TLED ambao umewezesha
wajasiriamali katika nyanja mbalimbali
ikiwemo soko, utoaji wa msaada wa mashine kwa ajili ya kuongeza tija
katika uzalishaji wa bidhaa, elimu ya biashara na utunzaji kumbukumbu pamoja na
misaada ya kifedha.
Naye
Mwenyekiti wa TWCC Mkoa wa Shinyanga, Joyce Egina alisema TLED inatakiwa kutoa mafunzo kwa vitendo ili kuzalisha watu
wengi na wajasiriamali waweze kukopesheka wenyewe pamoja na kuwapa
wanawake elimu ya kujitambua na
kujiamini kwani wengi wao wanakopa pesa kutoka vikundi mbalimbali na kushindwa kuendeleza biashara na matokeo
yake kufirisiwa.
Hata hivyo
mmoja wa wajasiriamali waliohudhuria sherehe hiyo, Herman Bundala aliliomba
shirika hilo kuboresha mfumo katika utoaji msaada wa mashine kwani wengi
wanazihitaji katika kuongeza ufanisi wa uzalishaji pamoja na waangalie namna ya
kuwawezesha ili wajifunze kwa vitendo.
No comments: