"Wananchi wanaendelea kunufaika na mfumo wa Ushirika"- Dkt. Tizeba
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
Waziri wa Kilimo Mhandisi Dkt. Charles
Tizeba akitoa taarifa ya ukusanyaji, Ukoboaji na uuzaji wa Kahawa mkoani Kagera
katika msimu wa mwaka 2018/2019 kwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Mhe. Kassim Majaliwa kwenye mkutano wa wadau wa Kahawa katika ukumbi wa ELCT
Mjini Bukoba.
Na Mathias Canal-WK, Bukoba-Kagera
Imebainika
kuwa pamoja na changamoto zilizojitokeza katika msimu wa kahawa wa mwaka
2018/2019 lakini bado mfumo wa uuzaji wa kahawa kupitia ushirika umekuwa wa
manufaa kwa mkulima kutokana na mkulima kupata uhakika wa kilo za kahawa
alizozipeleka chamani tofauti na ilivyokuwa hapo awali.
Manufaa hayo
yamejiri kutokana na kuingia mikataba ya kuuza moja kwa moja, ambapo matarajio
ya serikali ni kuhakikisha kuwa mkulima analipwa malipo ya awali na kiasi
kingine kubaki kwa ajili ya kuendelea kukusanya kahawa na kufanya maandalizi ya
malipo ya pili.
Waziri wa
Kilimo Mhandisi Dkt. Charles Tizeba amebainisha hayo leo wakati akitoa taarifa
fupi ya ukusanyaji, ukoboaji na uuzaji wa kahawa mkoani Kagera katika msimu wa
mwaka 2018/2019 kwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim
Majaliwa kwenye mkutano wa wadau wa kahawa.
Katika
mkutano huo uliofanyika kwenye Ukumbi ELCT Mjini Bukoba imeelezwa kuwa ubora wa
kahawa umeongezeka kwa kiasi kikubwa tofauti na misimu iliyopita.
Waziri
Tizeba alizitaja changamoto zinazovikabili vyama vya ushirika kwenye zao la
kahawa kwa msimu wa mwaka 2018/2019 kuwa ni pamoja na bei za mnadani, kahawa
kununuliwa kwa kiwango kidogo mnadani na wakati mwingine kutonunuliwa kabisa.
Kuwepo kwa
taarifa za upotoshaji kwa wakulima toka kwa walanguzi za kuzuia wakulima
kukusanya kahawa yao kupitia Vyama vya Ushirika vya Msingi kuwa wao
(Walanguzi) watanunua na kuwapatia bei
nzuri na kuwepo kwa katizo la umeme mara kwa mara linalopelekea ukoboaji wa
kahawa kutofanyika kwa wakati (hususani
wilayani Ngara).
Aidha
aliutaja mkakati wa kukabiliana na changamoto hizo kuwa ni pamoja na kuuza
kahawa kupitia mnada wa Moshi na mauzo ya moja kwa moja nje ya nchi “Direct
Export” ambao umeonesha kuwa na bei nzuri ukilinganisha na ile inayotolewa
mnadani Moshi na Kuomba mkopo wa nyongeza toka TADB kwa ajili ya kuwalipa
wakulima malipo yao ya Awali.
Alisema
Chama Cha Ushirika cha Karagwe KCU wanatarajiwa kupata mkopo wa Tshs. 2,000,000,000/=
kwa wiki hii na kiasi cha Tshs. 2,000,000,000/= kinaendelea kushughulikiwa ili
kiweze kutolewa wiki ijayo ambapo
wanatarajiwa kupata malipo ya mauzo ya kahawa yao kwa wiki ijayo kiasi cha Tshs
Bilioni 2.1
Mikakati
mingine ya kukabiliana na changamoto ya zao la kahawa ni pamoja na vyama
kuingia mikataba mbalimbali ya kuuza kahawa moja kwa moja nje. KDCU Ltd wana
mikataba ya mauzo nje yenye thamani ya Tshs 20,819,815,820.66 ambapo malipo
yake yanatarajiwa kulipwa kuanzia wiki hii. Kwa KCU Ltd wana mkataba wa Tshs
Bilioni 1.3 na wanatarajia kuingia mikataba mingine na wanunuzi wengine kwa
wiki ijayo.
Jitihada za
kupatikana kwa umeme wa uhakika katika kiwanda kilichoko wilayani Ngara
zinaendelea kufanyika kwa kushirikiana na mamlaka husika.
Katika hatua
nyingine alieleza kuwa mpaka sasa Kahawa iliyoko gharani ni Kiasi cha kilo
3,000,464 za kahawa maganda ambayo ilikuwa bado kukobolewa huku Kilo 8,191,867
za kahawa safi kilikuwa bado hakijauzwa na kilikuwepo kwenye maghala ya vyama.
Waziri Mkuu
Mhe. Kassim Majaliwa ameanza ziara ya kikazi mkoani Kagera kuanzia leo Oktoba
06 hadi Otoba 09, 2018 ambapo pamoja na mambo mengine lengo kuu la ziara hiyo
ni kukagua maendeleo ya zao la kahawa mkoani humu.
No comments: