Waziri Tizeba aipongeza MVIWATA kuwaunganisha pamoja wakulima
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
Waziri wa Kilimo Mhe. Mhandisi Dkt. Charles Tizeba akitoa
salamu za Wizara ya Kilimo mbele ya mgeni rasmi ambaye ni Waziri Mkuu wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa kwenye Maadhimisho ya
miaka 25 ya Mtandao wa Vikundi vya Wakulima Tanzania (MVIWATA) keo Oktoba 03, 2018 katika uwanja wa Jamhuri Mjini Morogoro.
Baadhi ya wakulima waliohudhuria maadhimisho hayo.
Naibu Waziri wa Kilimo Mhe. Omary Mgumba (Kushoto) aakisalimiana na
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa (Kulia)
Waziri wa Kilimo Mhe. Mhandisi Dkt. Charles Tizeba (kulia) akisalimiana
na Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Dkt. Bashiru Ally mara (kushoto).
Na Mathias Canal-WK, Morogoro
Waziri wa
Kilimo Mhe. Dkt Charles Tizeba ameupongeza Mtandao wa Vikundi vya Wakulima
Tanzania (MVIWATA) tangu kuanzishwa kwake mwaka 1993 kwa kuwa dira na muungano
wenye sauti moja yenye mshikamano na mafanikio makubwa kwa wakulima nchini.
Waziri
Tizeba ametoa pongezi hizo leo wakati akitoa salamu za Wizara ya Kilimo mbele
ya mgeni rasmi ambaye ni Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.
Kassim Majaliwa kwenye Maadhimisho ya miaka 25 ya mtandao huo.
Katika hafla
hiyo iliyohudhuriwa pia na Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Dkt. Bashiri
Ally, Waziri Tizeba alisema kuwa kipindi cha miaka 25 MVIWATA imekuwa mtandao
wenye dhamira chanya kwa kuwaunganisha wakulima wadogo kwa kutetea maslahi yao
na kujenga mikakati ya pamoja ya kujikwamua kijamii, kiuchumi na kiutamaduni.
Aliitaka
MVIWATA kuwa inapaswa kusimamia zaidi maslahi ya wakulima nchini kwa kuwa
wahusika wakuu na wamiliki wa mfumo wa uzalishaji na kuwa sehemu ya mfumo wa
maamuzi ya masuala yahusuyo maisha ya wakulima wadogo hususani mfumo wa
uzalishaji na rasilimali ardhi.
Dkt. Tizeba
aliwahakikishia wananchama hao zaidi ya 2000 walioshiriki katika kongamano hilo
la siku tatu kuwa wakulima wanapaswa kueleza changamoto mbalimbali
zinazowakabili ikiwa ni pamoja na kuzitafutia ufumbuzi wa haraka iwezekanavyo.
Mkurugenzi
Mkuu wa (MVIWATA, Stephen Ruvuga akisoma risala ya maadhimisho hayo aliipongeza
serikali katika kujenga uchumi wa Taifa katika kuimarisha sekta ya kilimo
nchini.
Alisema kwa
kutambua hilo hususani katika matumizi ya fedha za umma, kunapaswa kuongeza
msisitizo katika usimamizi wa matumizi ya fedha za umma na kuongeza ukusanyaji
wa mapato.
Alisema
pamoja na jitihada kubwa za serikali za kuimarisha sekta ya kilimo, wakulima
kwa ujumla bado wanachangamoto mbalimbali ikiwemo suala la ardhi, bei ya mazao
na soko la uhakika pamoja na mitaji ya uwezeshaji wakulima.
No comments: