Hatutamvumilia upotevu wa mapato serikalini- Nyongo
Wasiliana na BMG Blog/ BMG Online TV kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma ya Habari na Matangazo.
Naibu Waziri
wa Madini, Stanslaus Nyongo (katikati kwa waliokaa) akiwa katika picha ya
pamoja na waiohudhuria mafunzo hayo mara baada ya kufunga mafunzo ya
Kielektroniki ya ukusanyaji wa mapato ya Serikali mkoani Morogoro.
Naibu Waziri
wa Madini, Stanslaus Nyongo (wa tatu kulia) akiwa katika picha ya pamoja na
Viongozi waandamizi kutoka Wizara ya Madini na watendaji kutoka Chuo cha Mazimbu
Campus kilichopo mkoani Morogoro.
Naibu Waziri
wa Madini, Stanslaus Nyongo (katikati) wakijadiliana jambo na Mkurugenzi wa
Idara ya uhasibu, Anthony Tarimo (wa pili kushoto) mara baada ya kufika katika
chuo cha Mazimbu Campus kilichopo Mkoani Morogoro.
Mwakilishi
wa Chuo cha Mazimbu Campus cha Morogoro, Kundasen Swai akifafanua jambo kwa
Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (wa pili kulia).
Naibu Waziri
wa Madini, Stanslaus Nyongo akisaini kitabu cha wageni katika Ofisi ya Mkuu wa
Chuo cha Mazimbu Campus Mkoani Morogoro, anayeshuhudia ni Mkurugenzi wa Idara
ya Uhasibu, Anthony Tarimo.
Naibu Waziri
wa Madini, Stanslaus Nyongo akihutubia Wahasibu (hawapo pichani) wakati wakiwa
katika mafunzo ya Kielektroniki ya Ukusanyaji Mapato ya Serikali mkoani
Morogoro.
Mkurugenzi
wa Idara ya Uhasibu, Anthony Tarimo akihutubia Wahasibu (hawapo pichani) wakati
wa mafunzo ya Kielektroniki ya Ukusanyaji wa Mapato ya Serikalini mkoani
Morogoro.
Wahasibu
mbalimbali kutoka Wizara ya Madini pamoja na Wahasibu kutoka Tume ya Madini
wakimsikiliza Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (hayupo pichani) wakati
wa Mafunzo ya Kielektroniki ya Ukusanyaji wa Mapato ya Serikali.
Na Rhoda James- Morogoro
Naibu Waziri
wa Madini, Stanslaus Nyongo amewaeleza wahasibu wa madini nchini kuwa wizara
haitamvumilia mtu yeyote ambaye atakuwa chanzo cha upotevu wa ukusanyaji wa
mapato ya Serekali.
Nyongo
ameyasema hayo wakati akifunga Mafunzo ya Kielektroniki ya Ukusanyaji wa Mapato
ya Serikali ambayo yaliaanza tarehe 12 hadi 15 Novemba, 2018 katika Chuo cha
Mazimbu Campus kilichopo mkoani Morogoro.
Naibu Waziri
Nyongo amesema kuwa lengo la mafunzo hayo ni kuongeza tija na ufanisi katika
ukusanyaji wa mapato serikalini.
Akizungumza
katika Kikao hicho Nyongo alisema kuwa Viongozi wote wako tayari kutoa msaada
wowote masaa 24 hivyo kama kuna mhasibu ambaye atakuwa na uhitaji kwa masuala
ya kikazi asisite kuwasiliana nao waati wowote.
Aidha,
Nyongo alieleza kuwa tasnia ya uhasibu ni ya muhimu sana katika sekta ya
madini, hivyo ni vyema kila mmoja wetu kuhakikisha kuwa katika malengo yake
akahakikisha kuwa anafikiria lengo la ndani la Wizara la ukusanyaji wa Bilioni
500 linatimizwa.
Pamoja na
hayo, Nyongo alitoa pongezi kwa wahasibu wote kwa kufanikisha kufikia lengo la
wizara katika ukusanyaji wa mapato ya kiasi cha tsh Bilioni 310 kwa kipindi cha
mwaka 2017/2018 na kuwataka jitihada iliyotumika itumike katika kufanikisha
lengo la muhula huu wa fedha.
Aidha,
Nyongo amemtaka Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Shukurani Manya kuhakikisha
kuwakunakuwa na utekelezaji wa maazimio yote waliyoyafikia katika mkutano huo
ili kuweza kuboresha utendaji wao na kuongeza mapato ya wzara kwa mwaka wa
fedha 2018/19.
Akizungumzia
moja ya changamoto walizokuwa wakikutana nazo watumishi wa idara ya uhasibu,
Mkurugenzi wa Idara ya Uhasibu Athony Tarimo alisema ni katika uandaaji wa
ripoti ambayo kwa kupitia mafunzo hayo imepata utatuzi.
Aidha,
amemshukuru Naibu Waziri Stanslaus Nyongo kwa utayari wake wa kukubali kufunga
mafunzo hayo na kwamba anatumaini kwamba
wahasibu hao watakuwa mabalozi wazuri hasa katika kufundisha wengine ambao kwa
namna moja au nyingine hawakuweza kuhudhuria katika mafunzo hayo.
Mafunzo haya
yameshirikisha wahasibu wote wa Wizara ya Madini nchini kote na watumishi wa
takwimu kutoka Madini pamoja na watumishi kutoka Wizara ya Fedha na Mipango.
No comments: