Mbunge Biteko achangia miradi ya maendeo jimboni Bukombe
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma ya Habari na Matangazo.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Mbunge wa Jimbo
la Bukombe mkoani Geita, Doto Biteko (CCM), ameunga mkono juhudi za maendeleo
za wakazi wa Kata ya Namonge jimboni humo kwa kuchangia utekelezaji wa miradi
ya maendeleo iliyoanzishwa na wakazi hao.
Akizunguma
kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Shilabela Novemba 03,
2018, Biteko ambaye pia ni Naibu Waziri wa Madini alichangia mifuko 30 ya
saruji kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa darasa katika Shule ya Msingi
Shilabela pamoja na shilingi laki nane kwa ajili ya ujenzi wa choo katika Shule
ya Msingi Nyamagwangala.
Biteko alitumia
mkutano huo kuwapongeza wananchi wa Jimbo la Bukombe kwa kubuni na kutekeleza miradi
mbalimbali ya ya maendeleo na kwamba serikali itaendelea kuwaunga mkono kwani
maendeleo ni ushirika baina ya serikali na wananchi.
Mbunge wa Jimbo la Bukombe mkoani Geita, Doto Biteko (CCM) ambaye pia ni Naibu Waziri wa Madini, akizungumza na wakazi wa Kata ya Namonge kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Kijiji cha Shilabela.
Tazama BMG Online TV hapa chini
No comments: