Waziri Mkuu aweka jiwe la msingi mradi mkubwa wa maji wilayani Chato
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Matangazo.
Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa mradi wa maji mradi wa maji Imalabupina-Ichwankima wilayani Chato. Wanaoshuhudia ni Mkuu wa Mkoa Geita Mhandisi Robert Gabriel pamoja na Mwenyekiti wa CCM Mkoa Geita.
Kulia ni Mhandisi wa Maji wilayani Chato akitoa ufafanuzi wa mradi huo kwa Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa.
Kulia ni Mhandisi wa Maji wilayani Chato akitoa ufafanuzi wa mradi huo kwa Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa.
Mbunge wa Viti Maalum mkoani Geita, Vicky Kamata akisalimia wakati wa hafla ya uwekaji jiwe la msingi mradi wa maji Imalabupina-Ichwankima.
Mapema asubuhi kwenye mapokezi ya Mhe. Kassim Majaliwa katika uwanja wa ndege wa Chato
Burudani ya asili kutoka kikundi cha Bugobogobo
Burudani ya asili kutoka kikundi cha Bugobogobo
Na George Binagi, GB Pazzo-BMG
Waziri Mkuu
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa ameweka jiwe la msingi
kwenye ujenzi wa mradi wa maji Imalabupina-Ichwankima uliopo katika wilaya ya
Chato mkoani Geita.
Mhe.
Majaliwa ambaye ameanza ziara ya kikazi mkoani Geita leo Novemba 27, 2018, amesema
utaondoa kero ya maji kwa kwa wakazi wa wilaya ya Chato ikiwa ni utekelezaji wa
mpango wa serikali wa kumtua mama ndoo kichwani na hivyo kumtaka Mhandisi wa
Maji wilayani humo kuhakikisha mkandarasi anamaliza mradi huo kwa wakati.
Mhandisi wa
Maji wilayani Chato, amesema mradi huo unatarajiwa kukamilika mwakani mwezi
Februari na kuwahudumia wakazi wa Vijiji 11 ambapo hadi kukamilika kwake
utagharimu shilingi Bilioni 8.2.
Tazama BMG Online TV hapa chini
No comments: