Mama amshukru Rais Magufuli, amwongeza miaka 15
Wasiliana na BMG Blog/ BMG Online TV kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma ya Habari na Matangazo.
Mama Madina
Mbunda ambaye ni mkazi wa Katunguru wilayani Sengerema ametoa pongezi kwa Rais
Dkt. John Pombe Magufuli kwa namna anavyoendelea kuboresha sekta ya afya
ikiwemo ukarabati wa Vituo vya Kituo Afya kama vile Katunguru na kutaka
aendelee kuwa Rais hata baada ya muda wake kumalizika.
Mama Mbunda
alitoa kauli hiyo jana baada ya Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella kufanya ziara
katika Kituo cha Afya Katunguri kilichopewa shilingi Milioni 400 na Serikali kwa
ajili ya ujenzi wa majengo matano mapya ambayo ni nyumba ya mtumishi, maabara,
wadi ya wazazi, jengo la upasuaji pamoja na jengo la kuhifahia maiti kupitia
mfumo wa “Force Account”.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
No comments: