LIVE STREAM ADS

Header Ads

Mkuu wa Mkoa Mwanza afuta mapumziko ya Krismasi na Mwaka Mpya

Wasiliana na BMG Blog/ BMG Online TV kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma ya Habari na Matangazo.

Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella amefuta mapumziko ya Sikukuu za Krismasi na Mwaka Mpya 2019 kwa watumishi wa Halmashauri ya Buchosa wilayani Sengerema, baada ya ujenzi na ukarabati wa Kituo cha Afya Kome kutokamilika kwa wakati.

Mongella alitoa agizo hilo jana baada ya kufanya ziara katika Halmashauri ya Buchosa na kuagiza hadi kufikia Januari 10, 2019 atakaporudi katika Kituo cha Afya Kome akute ujenzi na ukarabati wake umekamilika.

Serikali ilitoa shilingi milioni 400 katika Kituo cha Afya Kome kwa ajili ya ukarabati na ujenzi wa majengo matano mapya ambayo ni nyumba ya mtumishi, maabara, wadi ya wazazi, jengo la upasuaji pamoja na jengo la kuhifahia maiti kupitia mfumo wa “Force Account”.
Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella (kushoto) akipokelewa na viongozi wa CCM na Serikali baada ya kuwasili katika Kituo cha Afya Kome, Halmashauri ya Buchosa wilayani Sengerema.
Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella (kushoto), akiwa ameambatana na Mkurugenzi Halmashauri ya Buchosa, Chrispin Luanda (kulia) pamoja na viongozi mbalimbali wakati akikagua ujenzi na ukarabati wa Kituo cha Afya Kome.
Miongoni mwa majengo mapya katika Kituo cha Afya Kome.
Jengo la chumba cha kuhifadhia maiti katika Kituo cha Afya Kome.
Nyumba ya mtumishi katika Kituo cha Afya Kome.
Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella (katikati), akiwa ameambatana na viongozi mbalimbali akiwemo Katibu Tawala Mkoa Mwanza, Christopher Kadio (kulia).
Tazama BMG Online TV hapa chini

No comments:

Powered by Blogger.