LIVE STREAM ADS

Header Ads

KaziNzuri: Mongella aagiza Mhandisi apandishwe cheo

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com

Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella amefanya ziara ya kukagua maendeleo ya ukarabati na ujenzi wa Kituo cha Afya Nyakaliro kilichopo Halmashauri ya Buchosa wilayani Sengerema na kuridhishwa na kasi iliyopo.

Kutokana na kasi hiyo, Mongella amemwagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Buchosa, Chrispin Luanda kumwandikia barua ya kumpandisha cheo Mhandisi anayesimamia ujenzi huo, Rahim Mgimba kuwa Kaimu Mkandarasi wa Halmashauri hiyo.

Mongella alitoa kauli hiyo jana Disemba 18, 2018 baada ya kufanya ziara katika Kituo hicho kilichopewa shilingi Milioni 400 na Serikali kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya mtumishi, maabara, wadi ya wazazi, jengo la upasuaji pamoja na jengo la kuhifahia maiti kupitia mfumo wa “Force Account”.
Ujenzi wa majengo mbalimbali katika Kituo cha Afya Nyakaliro wilayani Sengerema.
Tazama BMG Online TV hapa chini

No comments:

Powered by Blogger.