LIVE STREAM ADS

Header Ads

Mkuu wa Mkoa Mwanza akagua miradi ya maendeleo usiku

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com

Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Jana Disemba 18, 2018 Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella alifanya ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri ya Buchosa wilayani Sengerema, yenye hadhi ya Wilaya inayojengwa katika eneo la Isaka.

Mongella aliyekuwa na ziara ya kukagua miradi mbalimbali wilayani Sengerema alifika katika jengo la Hospitali hiyo jua likiwa limezama na akafarijika kuona ujenzi wake unaendelea vyema ambapo Serikali imetoa shilingi Bilioni 1.5 kwenye ujenzi huo.

Giza halikumzuia Mongella aliyekuwa ameambatana na viongozi na watendaji mbalimbali akiwemo Mkuu wa Wilaya Sengerema, Mwl. Emmanuel Kipole, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Buchosa, Chrispian Luanda pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama ngazi ya Wilaya na Mkoa, kwani majira ya saa mbili kasorobo usiku, alihitimisha ziara yake kwa akakagua ujenzi wa jengo la Halmashauri ya Buchosa ambalo ujenzi wake unagharimu shilingi Bilioni 2.5.

Wakazi Buchosa wana matumaini makubwa na miradi hii pamoja na mingine mingi hivyo matarajio yao ni kuona ikikamilika kwa wakati ili wapate huduma kikamilifu.
Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella (wa pili kulia), akikagua maendeleo ya ujenzi wa Ofisi za Halmashauri ya Buchosa wilayani Sengerema. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya hiyo, Mwl. Emmanuel Kipole na kulia ni Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Buchosa, Chrispin Luanda.
Tazama BMG Online TV hapa chini

No comments:

Powered by Blogger.