LIVE STREAM ADS

Header Ads

Manispaa ya Ilemela yajipanga kutekeleza vyema zoezi la ugawaji vitambulisho kwa wajasiriamali

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela mkoani Mwanza, John Wanga akizungumza kwenye kwenye kikao maalum/ cha dharura cha Baraza la Madiwani kilicholenga kujadili mapendekezo ya utekelezaji wa zoezi la ugawaji vitambulisho kwa wajasiriamali wadogo, hii leo Disemba 22, 2018.
Mhadhiri kutoka Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), Dkt. Nasibu Mramba akiwasilisha mada kwenye kikao maalum/ cha dharura cha Baraza la Madiwani kilicholenga kujadili mapendekezo ya utekelezaji wa zoezi la ugawaji vitambulisho kwa wajasiriamali wadogo.
Mhadhiri kutoka Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), Dkt. Nasibu Mramba akiwasilisha mada kwenye kikao maalum/ cha dharura cha Baraza la Madiwani kilicholenga kujadili mapendekezo ya utekelezaji wa zoezi la ugawaji vitambulisho kwa wajasiriamali wadogo.
Mratibu wa Sekta isiyo rasmi Manispaa ya Ilemela, Raphael Mphuru (kulia), akiwasilisha mapendekezo ya utekelezaji wa zoezi la ugawaji vitambulisho kwa wajasiriamali wadogo. Kushoto ni Mkurugenzi wa Shiriki la kutetea haki za wasichana na wanawake KIVULINI, Yassin Ally.
Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela, Renatus Mulunga (katikati), Kaimu Naibu Meya Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela, Alfred Wambura (kushoto) pamoja na Kaimu Mkurugenzi Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela, Shukrani Kyando (kulia), wakifuatilia mada wakati wa kikao maalum/ cha dharura cha Baraza la Madiwani kilicholenga kujadili mapendekezo ya utekelezaji wa zoezi la ugawaji vitambulisho kwa wajasiriamali wadogo.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Shirika la kutetea haki za wasichana na wanawake KIVULINI kwa kushirikiana na taasisi ya I4ID limewasilisha mapendekezo ya zoezi la ugawaji vitambulisho kwa wajasiriamali wadogo katika Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela mkoani Mwanza.

Mapendekezo hayo yamewasilishwa leo Disemba 22,2018 kwenye kikao cha dharura cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Ilemela, kabla ya zoezi hilo la ugawaji vitambulisho kwa wajasiriamali wadogo kuzinduliwa rasmi Alhamisi Disemba 27,2018.

Hatua hiyo imejiri baada ya Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela kuzishirikisha taasisi hizo kama mdau wa maendeleo katika Halmashauri hiyo lengo likiwa ni kuhakikisha zoezi hilo linakuwa na mafanikio makubwa hususani vitambulisho hivyo kuwafikia walengwa.

Miongoni mwa mapendekezo yaliyowasilishwa ni pamoja na uundaji wa Kamati Maalum ya kusimamia zoezi la ugawaji vitambulisho hivyo ambayo inajumuisha Watendaji wa Kata, Watendaji wa Mtaa, Polisi Kata, Maafisa Maendeleo, Maafisa Biashara, Viongozi wa Wajasiriamali wadogo (Mwenyekiti na Katibu), Mwakilishi wa Wajasiriamali Wanawake pamoja na Mwakilishi wa Wajasiriamali Vijana.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela, John Wanga pamoja na Mkurugenzi wa KIVULINI, Yassin Ally kwa pamoja wamesema lengo ni kuhakikisha zoezi hilo linafanikiwa na mafanikio makubwa na Halmashauri hiyo inakuwa ya mfano nchini kwa kutekeleza vyema zoezi la ugawaji vitambulisho vya wajasiriamali wadogo.
Tazama BMG Online TV hapa chini 

#PamojaDaimaBMG

No comments:

Powered by Blogger.