Kampuni ya Halotel yatoa SHUKRANI kwa wateja wake mkoani Mwanza
Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Katika
kusherehekea miaka mitatu tangu kuanza kutoa huduma zake hapa nchini, kampuni
ya mawasiliano ya simu Halotel imefanya tamasha kubwa na la wazi liitwalo “Shukrani
Music Concert” katika uwanja wa Furahisha Jijini Mwanza.
Tamasha hilo
limefanyika Januari 12, 2019 ambapo watumiaji wa mtandao wa Halotel walijipatia
zawadi mbalimbali ikiwemo simu za mkononi. Aidha kampuni hiyo pia ilitoa
mashuka 50 katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Mwanza Sekou Toure na mengine 50
katika Kituo cha Afya Bwisya wilayani Ukerewe.
Makamu
Mkurugenzi wa Halotel tawi la Mwanza linalojumuisha mikoa ya Mwanza, Shinyanga,
Simiyu na Mara, Francis Mafuru alisema kampuni hiyo iliyoanza kutoa huduma zake
hapa nchini Oktoba 15, 2015 pia imetumia zaidi ya shilingi Milioni Sita kununua
madawa na vifaa tiba kwa ajili ya Kituo cha Afya Bwisya pamoja na Hospitali ya
Sekou Toure.
Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella (kulia) ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye tamasha hilo akimkabidhi mwakilishi wa Mgangwa Mfawidhi wa Kituo cha Afya Bwisya, Cosmas Wanzara (kushoto), mashuka yaliyotolewa na kampuni ya Halotel.
Tamasha hilo lilipambwa na burudani kali kutoka kwa msanii Mr. Blue a.k.a BlueByser.
Tazama BMG Online TV hapa chini
No comments: