SHUKRANI MUSIC CONCERT: RC Mongella alivyompandisha Mr. Blue jukwaani
Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Wakazi wa
Jiji la Mwanza wamefurahia burudani kali kutoka kwa msanii wa muziki wa kizazi
kipya nchini, Mr. Blue kwenye tamasha la wazi la “Shukrani Music Concert”
lililoandaliwa na kampuni ya mawasiliano Halotel ikiwa ni sehemu ya kusherehekea
miaka mitatu tangu kuanzishwa kwake hapa nchini.
Katika
tamasha hilo lililofanyika Januari 12, 2018 kwenye uwanja wa Furahisha, kampuni
ya Halotel ilitoa zawadi mbalimbali kwa wateja wake ikiwemo fulana na simu. Pia
Halotel iliyoanza kutoa huduma zake nchini tangu Oktoba 15, 2015 ilitoa mashuka
50 katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Mwanza Sekou Toure na mengine 50 katika Kituo
cha Afya Bwisya wilayani Ukerewe. Pia ilitumia zaidi ya shilingi Milioni Sita
kununua madawa na vifaa tiba kwa ajili ya Kituo cha Afya Bwisya pamoja na
Hospitali ya Sekou Toure.
Mgeni rasmi
kwenye tamasha hilo alikuwa Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella ambapo mbali na
kuishukru kampuni ya Halotel kwa kuunga mkono juhudi za Serikali katika
kuboresha sekta ya afya nchini, pia alimpandisha jukwaani kwa shangwe msanii
Mr. Blue.
Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella akizungumza kwenye tamasha hilo.
Msanii Mr. Blue akipafomu kwenye tamasha hilo.
Shukrani Music Concert Jijini Mwanza
Tazama BMG Online TV hapa chini
No comments: