LIVE STREAM ADS

Header Ads

UWT Mwatulole mkoani Geita watoa pedi kwa wanafunzi wa kike

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com

Na Joel Maduka, Geita
Umoja wa Wanawake wa Chama cha Mapinduzi (UWT), tawi la Mwatulole Kata ya Buhala mkoani Geita, wamekabidhi taulo la zike (pedi) kwa wanafunzi wa kike katika Shule ya Sekondari Mwatulole.

Mwenyekiti wa tawi hilo, Rosemary Michael amesema taulo hizo zilipatikana kufuatia kongamano la wanawake lililofanyika hivi karibuni Mjini Geita na kwamba zitawasaidia wanafunzi wa kike wanaotoka katika familia zisizojimudu vyema kiuchumi na hivyo kuondokana na changamoto ya kukosa masomo wakati wa mzunguko wao wa hedhi.
Tazama BMG Online TV hapa chini

No comments:

Powered by Blogger.