Waziri Biteko akutana na kampuni ya Tanzaplus
Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Waziri wa Madini, Doto Biteko (kushoto) akizungumza na
watendaji wa kampuni inayojishughulisha na uyeyushaji wa madini ya bati katika
wilaya ya Kyerwa mkoani Kagera ya Tanzaplus. Waliokaa kutoka kushoto ni
Mkurugenzi wa Sera na Mipango kutoka Wizara ya Madini, Augustine Ollal, na
Upendo Fatukubonye na Hamis Mhando ambao ni watendaji kutoka kampuni ya
Tanzaplus.
Mkurugenzi kutoka kampuni ya Tanzaplus, Hamis Mhando (kulia)
akielezea jinsi teknolojia ya mfumo wa
usimamizi wa uzalishaji, usafirishaji na uuzaji wa madini inavyofanya kazi.
Waziri wa Madini, Doto Biteko akisisitiza jambo katika kikao
hicho.
Wataalam kutoka Wizara ya Madini wakinukuu maelekezo mbalimbali yaliyokuwa yanatolewa na Waziri wa Madini, Doto Biteko (hayupo pichani).
Waziri wa Madini, Doto Biteko jana amekutana na kampuni inayojishughulisha na uyeyushaji wa madini ya bati katika wilaya ya Kyerwa mkoani Kagera ya Tanzaplus katika Ofisi za Wizara ya Madini zilizopo jijini Dodoma.
Kikao chake pia kilishirikisha Mkurugenzi wa Sera na Mipango kutoka Wizara ya Madini, Augustine Ollal, Mhandisi Migodi Mkuu kutoka Tume ya Madini, Conrad Mtui pamoja na wataalam kutoka Wizara ya Madini.
Lengo la kikao hicho lilikuwa ni kampuni ya Tanzaplus Minerals kwa kushirikiana na kampuni nyingine ya AIMGROUP kutambulisha teknolojia ya mfumo wa usimamizi wa uzalishaji, usafirishaji na uuzaji wa madini.
Waziri Biteko aliitaka kampuni ya Tanzaplus kuendelea kufanya utafiti zaidi juu ya mfumo husika kwa kushirikisha wadau mbalimbali kabla ya kuwasilisha pendekezo lake Serikalini.
No comments: