LIVE STREAM ADS

Header Ads

Biteko afunguka kwa uchungu mkubwa mbele ya Makamu wa Rais

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Makamu wa Rais wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan jana ameendelea na ziara yake mkoani Tabora kwa kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo pamoja na kuzungumza na wananchi katika Wilaya za Uyui pamoja na Nzega.

Akiwa katika Wilaya ya Uyui, Mama Samia alikagua na kuweka jiwe la msingi kwenye ujenzi wa Kituo cha Afya Igalula na pia kuzungumza na wananchi ambapo kwa Wilaya ya Nzega, alikagua upanuzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Tabora (Kitete) unaogharimu shilingi Milioni 800, kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa kiwanda cha gesi cha Mara Moja Construction.

Pia alizungumza na wanachi kupitia mkutano wa hadhara katika Kata ya Puge na baadae kushiriki mazishi nyumbani kwa mbunge wa Nzega ambaye pia ni Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla aliyefiwa na mtoto wake.


Katika ziara hiyo iliyoanza juzi mkoani Tabora, Mama Samia aliambatana na viongozi mbalimbali wakiwemo Mawazili pamoja na Manaibu Mawaziri na hapa Waziri wa Madini, Doto Biteko alipata fursa ya kutoa salamu za wizara hiyo (video iko mwishoni).
Makamu wa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan akizungumza na wananchi kupitia mkutano wa hadhara.
Makamu wa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan akipanda mche wa mti baada ya kukagua upanuzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Tabora, Kitete.
Makamu wa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan pia aliungana na wananchi pamoja na viongozi mbalimbali kushiriki mazishi ya mtoto wa Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla (mbunge wa Nzega) yaliyofanyika nyumbani kwake Puge.
Tazama BMG Online TV hapa chini

No comments:

Powered by Blogger.