LIVE STREAM ADS

Header Ads

Waziri Biteko aweka jiwe la msingi ujenzi wa Kituo cha Pamoja cha Biashara ya Madini

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Waziri wa Madini, Doto Biteko akiweka Jiwe la Msingi katika Kituo Cha Pamoja Cha Biashara ya Madini. Pamoja naye ni Mbunge wa Simanjro, James Ole Millya, Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Prof.Simon Msanjila na Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro, Mhandisi Zephania Chaula.
Na Asteria Muhoza, Wizara ya Madini
Waziri wa Madini Doto Biteko akifuatilia jambo baada ya kuweka Jiwe la Msingi Kituo cha Pamoja Cha Biashara eneo la Mirerani. Wengine wa kwanza kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Alexander Mnyeti, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Dustan Kitandula. Kulia ni mwanzo ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini Prof. Simon Msanjila.
Waziri wa Madini Doto Biteko akizindua Jengo la Biashara na Uthaminishaji wa Madini, Mirerani. Wengine wanaoshuhudia ni Viongozi mbalimbali wa Mkoa, Wizara na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini.
Waziri wa Madini Doto Biteko Sambamba na Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Alexander Mnyeti pamoja na wageni waloshiriki hafla ya uzinduzi wa Jengo la Biashara na Uthaminishaji Madini, wakielekea mahali kunakojengwa Kituo cha Pamoja Cha Biashara ya Madini.
Jiwe la Msingi la Kituo cha Biashara ya Madini na Uthaminishaji Madini.




Description: https://mail.google.com/mail/u/0/images/cleardot.gif




Description: https://mail.google.com/mail/u/0/images/cleardot.gif
YALIYOJIRI WAKATI WA UZINDUZI WA JENGO LA BIASHARA, UTHAMINISHAJI NA UWEKEAJI JIWE LA MSINGI KITUO CHA PAMOJA CHA BIASHARA YA MADINI- MIRERANI, TAREHE 16 FEBRUARI, 2019

WAZIRI BITEKO ATAKA JENGO LA KITUO CHA PAMOJA CHA BIASHARA KUKAMILIKA IFIKAPO APRILI MWAKA HUU.

ASEMA ATAKAYEKAMATWA NA TANZANITE MARUFUKU KUINGIA TENA NDANI  YA UKUTA.

ATAKA MINADA YA TANZANITE ILIYOSIMAMISHWA SASA IANZE.

Ø SUMA JKT msitucheleweshe, ifikapo Aprili mwaka huu jengo liwe limekamilika. Jengo hili la Kituo cha Pamoja cha Biashara ya Madini litajengwa na SUMA JKT kwa gharama ya shilingi 1,148, 259,500.

Ø Tunafunga CCTV camera kuzunguka ukuta. Lengo la uwekaji wa mitambo hii ni kuimarisha ulinzi kwa ajili ya rasilimali na watu  waliomo na wanaoingia ndani ya ukuta. Tunataka tukiwa Dar es Salaam na Dodoma tuwaone. Rai yangu kwenu ni kila mtu awe mlinzi wa rasilimali madini na kwa upande wafanyabiashara wapende kununua katika mkondo sahihi madini yao ili kuepuka usumbufu.

Ø Tarehe 30 Januari 2019 nilisaini Kanuni za Mirerani Controlled Area. Nakuagiza Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro Kamati ianze kazi tuanze kusimamia Kanuni hizi.

Ø Tumekuja kumkabidhi mkandarasi site  hakuna kulala mpaka madini yalinufaishe taifa.

Ø Mkandarasi wa CCTV nakukabidhi kazi hii nataka ufanye kazi yenye ubora na kumaliza ndani ya Mkataba tuliokubaliana bila kuongeza hata sekunde.

Ø Tulieni tunakuja na utaratibu wa mashine. Wizi ni lazima  tuutoe kwenye fikra zenu.

Ø Wakati ukuta huu unajengwa  kulikuwa na siasa nyingi. Wapo waliouita jela lakini leo mapato yameongezeka mnalipa kodi vizuri. Tunakwenda kuondoa vikwazo kwenye biashara ya madini. Mtalipa mrabaha usiozidi asilimia 7. Deni limebaki kwenu.

Ø Suala kujengwa ukuta lilikuwepo tangu mwaka 2002 lakini haukujengwa. Ametokea mzalendo Rais Magufuli tumejenga. Asingekuwa yeye ingebaki hadithi nyingine.

Ø Nitawashangaa sana baada ya jitihada hizi tunazozifanya mapato yakishuka. Mkuu wa Mkoa wasimamieni hawa  huku mkiwalea.

Ø Jengo la biashara ya madini limejengwa mahususi ili kurahisisha uthaminishaji wa madini pindi yanapovunwa hapa ndani.Ma broker tumewajengea nyumba hii hapa tuheshimu taratibu.

Ø Jengo hili la biashara na uthaminishaji litatumika kuwakutanisha wafanyabiashara wadogo na wenye madini ili kuweza kufanya biashara sehemu salama na  kwa uwazi. Kama alivyosema Katibu Mkuu, jengo hili limegharimu shilingi milioni 85.

Ø Tanzania Tumegeuka kuwa darasa kwa jirani zetu  na nchi nyingine kutokana na namna tunavyosimamia Sekta ya madini. Watu wa mataifa wanakuja kujifunza lakini pia Tunapata mialiko mingi kutoka nchi mbalimbali ili tuwaeleze namna tunavyosimamia rasilimali hii.

Ø Tutumie madini yetu kubadilisha maisha yetu. Tunataka siku moja watoto wa Simanjiro wasome kwenye shule nzuri, watumie barabara nzuri, akina mama wapate huduma za afya sehemu nzuri. Haya ndiyo mambo tunayoyataka. Siasa nyingine siyo agenda ya watanzania.

Ø Tanzania ni nchi ya 3 Afrika kwa kuzalisha dhahabu, ya pili Afrka kwa madini ya vito na ya 18 duniani kwa kuzalisha dhahabu lakini utajiri huu wa madini na maisha ya watanzania havifanani.

Ø Minada ya Tanzanite iliyosimamishwa sasa ianze.

Ø Chama Cha MAREMA unganeni,tukigundua hamna msaada tutawaacha.

Ø Hatutaki kukwamishana,tunataka kusimamia sekta..Wachimbaji acheni majungu, toeni taarifa za kweli.

Ø Hatutawatoza fedha nyingi lakini mtatuonesha vitambulisho. Natoa maelekezo kuanzia leo tozo za kiingilio zitatozwa kwa wale wanaofanya kazi. Ndani ya mgodi watalipa shilingi elfu 50,000 kwa mwaka, Mabroker watalipa shilingi elfu 30,000 kwa mwaka na wana Appolo, wafanyabiashara wadogo kama wachekechaji, mama lishe watalipa shilingi 20,000 kwa mwaka.

Ø Naomba Wizara ya Kazi kupitia Mfuko wa fidia kwa wafanyakazi  ( WCF) na  Mifuko ya Hifadhi ya Jamii kuja kujifunza na kutengeneza muundo ambao unaendana na aina ya kundi hili ili kuweza kulihudumia kundi hili la wachimbaji wadogo wa madini.

Ø Katika mkutano wa wadau wa tarehe 22 Januari, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli  pamoja na mambo mengine alisisitiza kuimarisha mazingira ya ufanyaji biashara ya Madini Tanzania na pia kuimairisha usalama. Tuliagizwa kiualisia kuanza mara moja kuweka mifumo ya kidigitali kuzunguka ukuta.

ALIYOYASEMA MKUU WA MKOA WA MANYARA, ALEXANDER MNYETI

Ø Mkoa wa Manyara ni mkoa mkubwa wenye Tanzanite ambayo haipo  popote duniani. Unapokuwa Mkuu wa Mkoa kama huu lazima uweze kudhibiti Tanzanite. Nataka nikamwambie Mhe. Waziri  tuna madini mengi zaidi ya Tanzanite.

Ø Kwenye madini lazima nibanane na wewe. Nisipodhibiti sina cha kumwambia Mhe. Rais. Tutapambana mpaka dakika ya mwisho kuhakikisha kodi zinapatikana. Babati tuna rubi ya kutosha. Nataka nikwambie ifanye Babati kuwa Makao Makuu ya Madini nchi nzima.

Ø Mhe. Waziri kazi yetu ni kusimamia mnayoyapitisha juu ili yasipotoshwe na yatekelezwe kwa Mujibu wa Sheria.

Ø Mhe. Rais alituelekeza tupitie na kukubaliana kuweka mazingira mazuri ya kuboresha Tanzania kupitia sekta hii. Tulikaa kujadili mabadiliko makubwa. Nina hakika mabadiliko makubwa yanakuja.

Ø Mhe. Waziri tumeshakubaliana na wadau hawa mambo mengi. Tunataka kuona mengi kutoka kwao.

Ø Ni matarajio yangu kuwa shughuli nyingi zitafanyika ndani ya jengo la Kituo cha Biashara.

Ø Nakipongeza Chama Cha Marema kwa kufanya kazi nzuri. Ukipingana na Serikali hakuna unachoweza kufanya. Hakuna aliye juu ya serikali.

ALIYOYASEMA MWENYEKITI WA  KAMATI YA KUDUMU YA  BUNGE YA NISHATI NA MADINI, DUSTAN KITANDULA

Ø Mhe. Rais ameonesha uungwana, mpira uko kwenu. Hisani pekee kwake ni ninyi kulipa kwa kuonesha kwa vitendo. Yale yaliyokuwa yakiwakwaza yameondoka, mlipe kodi.

Ø Tumewaona mkiwa katika maandamano ya kumuunga mkono Rais. Kikao cha Januari 22 kilionesha dhamira ya Rais na aliahidi kutekeleza  kero zenu ndani ya kipindi kifupi. Tuliletewa miswada kufanya mabadiliko.

Ø Nampongeza Rais kwa kuondoa vikwazo kwa wachimbaji wadogo. Serikali imedhamiria kuhakikisha sekta hii inalinufaisha taifa.

ALIYOYASEMA MBUNGE WA SIMANJIRO, JAMES OLLE  MILLYA

Ø Kuwepo kwa ukuta huu hakumaanishi hakuna majirani. Kwa mujibu wa Sheria na  taratibu zake  nakuomba  Mhe  Waziri migodi hii isaidie jamii. Wanaofanya uchimbaji wakumbuke vijiji vya jirani.

Ø Baada  ya kujengwa ukuta bado wanapanga mistari mirefu. Wanaongia ndani wakaguliwe mapema.

Ø Bado kuna changamoto kwako Mhe. Waziri na  Katibu Mkuu ikiwezekana muwaletee maji.

ALIYOYASEMA MWENYEKITI WA MAREMA, JUSTIN NYARI

Ø Mhe. Rais ameweka alama ambayo haitapotea, alama ambayo itakumbukwa kwa vizazi na vizazi.

Ø Ujenzi wa kituo cha pamoja cha biashara ni  mwanzo mzuri kwetu na mkoa wetu na nchi yetu, wachimbaji wako tayari kushirikiana na serikali.

No comments:

Powered by Blogger.