LIVE STREAM ADS

Header Ads

Wanahabari wahimizwa kushiriki kwenye hatua za utungaji sheria

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Mwezeshaji, Sengiyumva Gasirigwa akizungumza kwenye mafunzo ya siku mbili kuanzia jana kwa waandishi wa habari kutoka mikoa ya Mwanza, Mara na Simiyu yenye lengo la kuwajengea uwezo kuhusu sheria mpya za habari. Mafunzo hayo yanafanyika Mjini Bariadi yakiandandaliwa na Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika MISA tawi la Tanzania kwa kushirikiana na Internews ofisi ya Tanzania.

“Lengo la mafunzo haya ni kubadilishana uzoefu, kukumbushana kwamba kuna sheria za vyombo vya habari, upatikanaji wake ulikuwaje, zinatunufaisha kwa kiwango gani na zina vikwazo gani kwetu wanahabari”. Alisisitiza Sengiyumva Gasirigwa ambaye ni Mwezeshaji wa mafunzo hayo na kuongeza;

“Waandishi wa habari mnao wajibu wa kushiriki kwenye michakato ya upatikanaji wa sheria za vyombo vya habari  kuanzia kwenye utungaji wake na hata maboresho ya sheria hizo pamoja na kanuni zake ikizingatiwa kwamba michakato hiyo ni endelevu”.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Mshiriki, Aidan Mhando akichangia mada kwenye mafunzo hayo.
Mshiriki Dinna Maningo akifafanua jambo kwenye mafunzo hayo.
Washiriki wa mafunzo hayo wakimsikiliza mshiriki mwenzao, Dinna Maningo wakati akifafanua jambo kwenye mafunzo hayo.
"Energizing session"
“Kipindi cha uchaguzi ni kipindi muhimu sana kwetu wanahabari ambapo tunahitaji kufanya kazi kwa ushirikiano na watoa taarifa wetu hivyo mafunzo haya yatawaongeza kiwango cha uelewa kuhusu sheria za vyombo vya habari ikiwemo Sheria ya Haki ya Kupata Taarifa ya mwaka 2016 ili kuboresha utendaji kazi wenu katika chaguzi zijazo”. Sengiyumva Gasirigwa, Mwezeshaji mafunzo kwa waandishi wa habari kutoka mikoa ya Mara, Mwanza na Simiyu yaliyoandaliwa na MISA Tanzania kwa kushirikiana na Internews.
“Waandishi wa habari tunao wajibu wa kushiriki kwenye michakato ya upatikanaji wa sheria za vyombo vya habari  kuanzia kwenye utungaji wake na hata maboresho ya sheria hizo pamoja na kanuni zake ikizingatiwa kwamba michakato hiyo ni endelevu”.  Sengiyumva Gasirigwa, Mwezeshaji mafunzo kwa waandishi wa habari kutoka mikoa ya Mara, Mwanza na Simiyu yaliyoandaliwa na MISA Tanzania kwa kushirikiana na Internews.
Tazama BMG Online TV haoa chini

No comments:

Powered by Blogger.