LIVE STREAM ADS

Header Ads

Ilivyokuwa Uzinduzi wa Jukwaa la "SITETEREKI" Jijini Mwanza

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Kaimu Katibu Tawala mkoani Mwanza, Emily Kasagara (wa kwanza kulia) pamoja na viongozi mbalimbali wakizindua jukwaa la mawasiliano ya afya liitwalo Sitetereki. Uzinduzi wa jukwaa hili lililo chini ya mradi wa USAid Tulonge Afya pamoja na Wizara ya Afya ulifanyika Machi 07, 2019 Jijini Mwanza kwa kujumuisha mikoa ya Kanda ya Ziwa.

Mwakilishi kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kitengo cha Elimu ya Afya kwa Umma, Dkt. Tumain Haonga alisema jukwaa la Sitetereki linawalenga zaidi vijana kuanzia miaka 15 hadi 24 katika kutekeleza afua mbalimbali za afya ili kupambana na vifo vitokanavyo na uzazi.


Afua hizo zitasaidia kupunguza vifo vya akina mama wakati wa kujifungua kutoka vifo 556 kwa kila vizazi 100,000 kwa mwaka hadi kufikia vifo 292 ifikapo mwaka 2020.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Mgeni rasmi, Kaimu Katibu Tawala mkoani Mwanza, Emily Kasagara akisisitiza jambo baada ya uzinduzi wa jukwaa la Sitetereki kwa mikoa ya Kanda ya Ziwa uliofanyika Jijini Mwanza.
Mgeni rasmi akiwa kwenye picha ya pamoja na wawakilishi/ wadau kutoka taasisi mbalimbali.
Mgeni rami, viongozi mbalimbali na wanahabari Jijini Mwanza wakiwa kwenye picha ya pamoja.
Mgeni rasmi akiwa kwenye picha ya pamoja na wawakilishi/ wadau kutoka taasisi mbalimbali.
Kumbukumbu na mgeni rasmi.
Mgeni rasmi akiwa kwenye picha ya pamoja na wawakilishi/ wadau kutoka taasisi mbalimbali.
Kumbukumbu kupitia zuria jekundu la Sitetereki pia zilikuwepo.
Washiriki wa warsha ya uzinduzi wa jukwaa la Sitetereki kutoka mikoa ya Kanda ya Ziwa.
Washiriki wa warsha hiyo.
Baada ya uzinduzi huo, wadau walijadiliana namna ya kutekeleza afua mbalimbali katika kupambana na changamoto za uzazi na baada ya majadiliano, ukafuatia wasaa wa maakuli.
Tazama BMG Online TV hapa chini
#PamojaDaimaBMG

No comments:

Powered by Blogger.