LIVE STREAM ADS

Header Ads

Zoezi la ugawaji bure vyandarua mashuleni lazinduliwa mkoani Mwanza

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella amezindua rasmi zoezi la ugawaji bure vyandarua vyenye dawa ya kuua mbu kwa wanafunzi wa Shule za Msingi ikiwa ni sehemu ya utekelezaji afua mbalimbali za kupambana na Malaria.

Uzinduzi huo umefanyika Oktoba 10, 2019 katika Shule ya Msingi Nyanza jijini Mwanza ambapo jumla ya Shule za Msingi 976 mkoani Mwanza zitafikiwa na zoezi hilo litakalodumu kwa muda wa wiki mbili kuanzia tarehe 09-23 Oktoba, 2019.
Tazama BMG ONLINE TV hapa chini

No comments:

Powered by Blogger.