LIVE STREAM ADS

Header Ads

Tamasha la Urithi kutikisa jijini Mwanza kwa siku tatu mfululizo

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Majaliwa Kasim Majaliwa anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye kilele cha Tamasha la Urithi (Urithi Festival 2019) litakalofanyika katika viunga vya Rock City Mall jijini Mwanza.

Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella ameyasema hayo Oktoba 29, 2019 wakati akitoa taarifa kwa vyombo vya habari kuhusiana na tamasha hilo litakalofanyika kwa siku tatu mfululizo kuanzia Oktoba 31 hadi Novemba 02, 2019.


Tamasha la pili la Urithi wa Utamaduni wa Mtanzania (Urithi Festival) lilizinduliwa rasmi Septemba 22, 2019 na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan jijini Dar es salaam na kisha kuzunguka mikoa mbalimbali nchini kabla ya kuhitimishwa jijini Mwanza.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
 Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella akitoa taarifa kuhusu tamasha la Urithi 2019 litakalofanyika jijini Mwanza.
Tazama BMG TV ONLINE hapa chini

No comments:

Powered by Blogger.