LIVE STREAM ADS

Header Ads

RC Mongella azindua mradi mkubwa wa maji katika Shule za Lake Mwanza

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com

Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella (wa tano kushoto) amezindua mradi wa maji ya kisima kirefu chenye urefu wa zaidi ya mita 100 katika Shule za Lake jijini Mwanza uliogharimu milioni 18 hadi kukamilika.

Mradi huo umefadhiliwa na taasisi ya kidini ya “Siri Guru Singh Sabha Mwanza” ukielezwa kwamba utaleta manufaa makubwa ikiwemo kupunguza gharama za ankra za maji ambazo kwa mwezi zilikuwa kati ya shilingi milioni tatu hadi milioni tano kwa mwezi.

Akizungumza na uongozi pamoja na wanafunzi wa Shule za Lake kabla ya kuzingua mradi huo Novemba 16, 2019 Mongella ametaka Shule hiyo kurejea kwenye enzi zake ambapo ilikuwa ikifanya vizuri katika mitihani ya kitaifa ili kuendana na sifa yake ya kutoa wanafunzi bora ambao sasa ni viongozi mashughuli nchini akiwemo Rais Dkt. John Pombe Magufuli.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
 Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella akizungumza kwenye hafla.
 Meneja wa Shule za Lake Mwanza, Jagdish Mehta akitoa salamu kwenye hafla hiyo.
 Viongozi mbalimbali wakiwemo wawakilishi wa Bodi ya Wamiliki pamoja na wafadhili kutoka taasisi Siri Guru Singh Sabha Mwanza.
 Wazazi, waalimu na wanafunzi wakifuatilia hafla hiyo.
 Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella (wa tano kushoto) akikata utepe kuashiria uzinduzi wa mradi wa maji.
 Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella akiweka jiwe la msingi kwenye mradi huo.
Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella akionja maji ya kisima hicho ambayo ni safi na salama.
Tazama BMG TV ONLINE hapa chini

No comments:

Powered by Blogger.