LIVE STREAM ADS

Header Ads

Viongozi UWT watakiwa kuacha ubinafsi

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Viongozi wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) wametakiwa kuacha ubinafsi na badala yake wazidi kushirikiana na wanachama wa umoja huo ili kufanikisha ushindi wa CCM katika Uchaguzi Mkuu 2020.

Rai hiyo ulitolewa Januari 04, 2019 na mmoja wa waasisi wa UWT nchini, Balozi Getrude Mongella wakati akizungumza kwenye kikao cha Kamati Tendaji ya umoja huo ngazi ya Mkoa Mwanza.

Kauli hiyo iliungwa mkono pia na Mwenyekiti wa UWT Mkoa Mwanza, Hellen Bogohe aliyesema ubinafsi miongoni mwa baadhi ya viongozi wa UWT umekuwa kikwazo kwa wanawake kuchaguliwa kwenye nafasi mbalimbali za uongozi.
Tazama BMG TV hapa chini

No comments:

Powered by Blogger.