LIVE STREAM ADS

Header Ads

Kufikia Uchumi wa Viwanda "vyuo vyatakiwa kuandaa mitaala inayotoa ujuzi"

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
 Vyuo vya Maendeleo ya Jamii na Ufundi Tanzania vimetakiwa kuandaa mitaala inayotoa ujuzi na stadi muhimu zinazohitajika katika soko la ajira ikiwemo viwanda ili kuwawezesha wahitimu wake kujiajiri na kuajiri watu wengine.

Mkurugenzi na Msajili wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali, Vickness Mayao aliyasema hayo Februari 24, 2020 jijini Mwaanza wakati akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. John Jingu kwenye kongamano la wadau Kanda ya Ziwa kujadili utekelezaji wa dhana ya Uanagenzi.

Mayao alisema Uanagenzi ni dhana inayolenga kuimarisha ujuzi kwa wahitimu hivyo kongamano hilo lililowahusisha wadau mbalimbali wakiwemo waajiri kutoka taasisi binafsi na za Serikali litasaidia kupata mikakati ya pamoja ya kutekeleza vyema dhana hiyo.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
 Mkurugenzi na Msajili wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali, Vickness Mayao akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. John Jingu kwenye kongamano la wadau Kanda ya Ziwa kujadili namna ya kutekeleza dhana ya Uanagenzi.
 Viongozi mbalimbali meza kuu akiwemo mgeni rasmi Mkurugenzi na Msajili wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali, Vickness Mayao (katikati) aliyemwakilisha Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. John Jingu kwenye kongamano la wadau kujadili utekelezaji wa dhana ya Uanagenzi.
 Wadau na Wataalamu wa Maendeleo ya Jamii Kanda ya Ziwa wakiwa kwenye kongamano la kujadili namna ya kutekeleza dhana ya Uanagenzi.
 Wataalamu wa Maendeleo ya Jamii Kanda ya Ziwa wakiwa kwenye kongamano hilo.
 Wadau mbalimbali waliohudhuria kongamano la kujadili namna ya kutekeleza dhana ya Uanagenzi Kanda ya Ziwa.
Tazama BMG TV hapa chini

No comments:

Powered by Blogger.