Biteko akagua miradi ya maendeleo Bukombe
Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Mbunge wa
Jimbo la Bukombe, Doto Biteko ambaye pia ni Waziri wa Madini akizungumza na
wakazi wa Kata ya Uyovu jimboni humo Februari 28, 2020 kupitia mkutano wa
hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Buganzu.
Kabla ya
mkutano huo, Biteko alikagua miradi mbalimbali ya maendeleo na kuwapongeza
wananchi kwa kushirikiana kutekeleza miradi hiyo ikiwemo ujenzi wa vyumba vya
madarasa na kuanzisha ujenzi wa Shule.
Baadhi ya wakazi wa Kata ya Uyovu jimboni Bukombe wakimsikiliza mbunge wao, Doto Biteko (hayuko pichani) ambaye pia ni Waziri wa Madini.
Mbunge wa Jimbo la Bukombe mkoani Geita, Doto Biteko ambaye pia ni Waziri wa Madini alifika kukagua ujenzi wa Shule mpya ya Msingi Lyobaika ambayo ujenzi wake umeanzishwa na wananchi.
Mbunge wa Jimbo la Bukombe mkoani Geita, Doto Biteko ambaye pia ni Waziri wa Madini pia alikagua ujenzi wa Shule mpya ya Msingi Kapwani inayojengwa kwa nguvu za wananchi.
Mbunge wa Jimbo la Bukombe mkoani Geita, Doto Biteko ambaye pia ni Waziri wa Madini aliunga mkono juhudi za wananchi kwa kuahidi kuwasaidia ili kukamilisha miradi hiyo na mingine mingi jimboni Bukombe.
Tazama BMG TV hapa chini
SOMA>>> Habari zaidi kutoka Bukombe
No comments: