Halmashauri mkoani Mwanza zabanwa ukusanyaji mapato/ imo Ukerewe iliyoshika mkia
Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Mkuu wa Mkoa
Mwanza, John Mongella akizungumza kwenye kikao cha pili cha Kamati ya Ushauri (RCC) kwa mwaka wa fedha 2019/2020 kilichoketi Machi 07, 2020 kujadili ajenda mbalimbali ikiwemo utekelezaji wa
maazimio ya kikao kilichopita, mapendekezo ya bajeti ya Mkoa, gharama za
uendeshaji wa mfumo wa Serikali kimkoa pamoja na bajeti ya miradi ya maendeleo
kimkoa.
Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella (kulia) alitumia kikao hicho kusisitiza Halmashauri zote mkoani Mwanza kuongeza ukusanyaji wa mapato hadi kufikia asilimia 75 mwezi Aprili mwaka huu ikiwemo Halmashauri ya Ukerewe ambayo ilishika nafasi ya pili kutoka mwisho katika ukusanyaji wa mapato kwa mwaka wa fedha uliopita.
Katibu Tawala Mkoa Mwanza, Emmanuel Tutuba akitoa salamu zake kwenye kikao hicho.
Viongozi mbalimbali wakiwemo Wakuu wa Wilaya walioshiriki kikao hicho.
Viongozi mbalimbali wakiwemo Wabunge walioshiriki kikao hicho.
Tazama BMG TV hapa chini
SOMA>>> Habari kuhusiana na Ukerewe
No comments: