LIVE STREAM ADS

Header Ads

MWANZA- Fuatilia ujenzi wa Soko la Kisasa Kiloleli

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com

Baada ya kufanya utafiti na kubaini wafanyabiashara wadogo hususani wanawake wanakabiliwa na mazingira magumu ya kufanyia biashara, shirika la kutetea haki za wanawake na wasichana (KIVULINI) limesaidia upatikanaji wa fedha kwa ajili ya uboreshaji wa soko la Kiloleli lililopo Wilaya Ilemela pamoja na Mirongo katika Wilaya ya Nyamagana.

Uboreshaji wa masoko hayo unahusisha ujenzi na ukarabati wa miundombinu bora na rafiki kibiashara ikiwemo vyoo, mitaro ya kuzuia maji kuingia sokoni, eneo maalumu kwa watoto kuchezea na akina mama kunyonyeshea pamoja na Kituo cha daladala Kiloleli.

Soko la Kiloleli linatarajiwa kugharimu shilingi Milioni 127 ikiwa ni pamoja na miundombinu iliyotajwa hapo juu huku soko la Mirongo likigharimu shilingi Milioni 90.8 ambapo ujenzi huo unatarajiwa kukamilika katika kipindi cha miezi mitatu kuanzia mwezi Februari 2020.
Ungana na BMG TV kutazama hatua ulipofikia ujenzi, ukarabati na uboreshaji wa soko la Kiloleli.

No comments:

Powered by Blogger.