Serikali yaboresha vitambulisho vipya vya machinga
Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Serikali imefanya maboresho ya vitambulisho vipya vya wafanyabiashara wadogo ikiwemo kila Mkoa kuwa na namba maalum ya utambulisho (serial number) lengo likiwa ni kuondoa baadhi ya dosari zilizobainika kwenye vitambulisho vya hapo awali.
Hayo yalielezwa Mei 19, 2020 wakati Mkuu wa Mkoa Mwanza John Mongella akikabidhi vitambulisho elfu 15 vya wafanyabishara wadogo kwa Wakuu wa Wilaya ikiwa ni awamu ya kwanza kwa mwaka huu 2020.
#BMGHabari
Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella (kulia) akimkabidhi vitambulisho vya machinga Mkuu wa Wilaya Misungwi, Juma Sweda (kushoto).
Mkuu wa Wilaya Kwimba, Senyi Ngaga (kushoto) akipokea vitambulisho vya machinga.
Mkuu wa Wilaya Magu, Dkt. Philemon Sengati (kushoto) akipokea vitambulisho vya machinga.
Mkuu wa Wilaya Sengerema, Dkt. Emmanuel Kipole akipokea vitambulisho vya machinga.
Mkuu wa Wilaya Ilemela, Dkt. Severine Lalika akipokea vitambulisho vya machinga.
Tazama BMG TV hapa chini
No comments: