Wakusanya ushuru Ukerewe wasakwa “warejeshe Milioni 274”
Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Mkuu wa Mkoa
wa Mwanza, John Mongella ameagiza kukamatwa kwa wakusanya ushuru watano katika
Halmashauri ya Wilaya Ukerewe wanaotuhumiwa kuhusika na upotevu wa shilingi
milioni 274.6 pamoja na mashine tano za kukusanyia ushuru (POS).
Mongella
ametoa agizo hilo kwa Mkuu wa Polisi Wilaya Ukerewe pamoja na Mkuu wa TAKUKURU
wilayani humo kuwakamata watuhumiwa hao ambao ni Leopard Musiba, Fortunatus
Mutesigwa, Thomas Bagetilanya, Frola Ntale na Didas Majura ili ndani ya wiki
moja wawe wamerejesha fedha hizo.
Mongella
alitoa agizo hilo Juni 04, 2020 wakati akizungumza kwenye kikao cha baraza la
madiwani wa Halmashauri ya Ukerewe cha kujadili hoja za Mkaguzi na Mdhibiti
Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2018/19.
Tazama BMG ONLINE TV hapa chini
SOMA>>> Habari kutoka Ukerewe
No comments: