Serikali yajiweka kando bei ya Pamba
Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Serikali
imesema haitajihusisha tena na upangaji wa bei ya zao la pamba na badala yake
bei hiyo tapangwa na wakulima pamoja na wanunuzi wa zao hilo kulingana na
mwelekeo wa soko la dunia.
Waziri wa
Kilimo, Japhet Hasunga aliyasema hayo Juni 07, 2020 wakati akizungumza kwenye
mkutano wa wadau wa pamba uliofanyika jijini Mwanza ukihusisha washiriki kutoka
mikoa 13 inayolima zao hilo.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga akizungumza kwenye mkutano huo.
Mwakilishi wa wanunuzi wa Pamba, Christopher Gachuma akitoa salamu zake kwenye mkutano huo.
Tazama BMG ONLINE TV hapa chini
SOMA>>> Habari mbalimbali za Pamba
No comments: