Biteko aupiga ‘STOP’ mgodi wa GGM
Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Waziri wa Madini, Doto Biteko amekataa ombi la mgodi wa dhahabu
wa GGML uliopo mkoani Geita, kumtumia mkandarasi kutoka nje ya nchi kwa ajili ya
ujenzi mfumo wa kupokelea umeme wa TANESCO katika mgodi huo.
Biteko aliyasema hayo Julai Mosi 2020 alipotembelea mgodi huo na kueleza kuwa msimamosi wa Serikali ni kuona kazi hiyo ikifanywa na mkandarasi mzawa huku matumizi ya umeme wa TANESCO yakianze mapema badala ya matumizi ya mafuta kwani hatua hiyo itapunguza gharama za uendeshaji kwa zaidi ya asilimia 50.
Na George Binagi-GB Pazzo
Waziri wa Madini, Doto Biteko akizungumza na Menejimenti ya mgodi wa GGML alitembelea mgodini hapo Jumatano Julai Mosi 2020.
Waziri wa Madini, Doto Biteko akizumgumza na menejimenti ya mgodi wa GGM.
Mkuu wa Mkoa Geita, Mhandisi Robert Gabriel akisisitiza umuhimu wa wazawa kushiriki kwenye shughuli mbalimbali za kibiashara katika mgodi wa GGML.
Tazama BMG ONLINE TV hapa chini
No comments: