LIVE STREAM ADS

Header Ads

MWANZA “Serikali yasitisha mkataba na mkandarasi wa umeme vijijini”

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Serikali kupitia Wakala wa Usambazaji Umeme Vijini (REA) imevunja mkataba na Mkandarasi kampuni ya NIPO Group iliyokuwa ikisambaza umeme katika Vijiji mbalimbali mkoani Mwanza.

Maamuzi hayo yameridhiwa kwenye kikao cha Bodi ya Wakurugenzi wa REA kilichoketi Jumatatu Agosti 03, 2020 jijini Mwanza baada ya kuelezwa kuwa Mkandarasi huyo ameshindwa kutekeleza vyema na kwa wakati majukumu yake.

Kufuatua hatua hiyo, kampuni ETDCO ambayo ni kampuni tanzu ya Shirika la Umeme nchini (TANESCO) imepewa majukumu hayo ya kusambaza umeme katika Vijiji 70 mkoani Mwanza ambavyo havikufikiwa na kampuni ya NIPO Group kupitia mradi wa REA awamu ya tatu mzunguko wa kwanza ambao utekelezaji wake unaendelea.

Tazama BMG ONLINE TV hapa chini

SOMA>>> Habari mbalimbali

No comments:

Powered by Blogger.