Wanahabari watakiwa kuchangamkia fursa NHIF
Mkurugenzi Mkuu
wa NHFI, Benard Konga aliyasema Septemba 14, 2020 jijini Mwanza wakati
akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi rasmi wa mpango wa Bima ya Afya kwa kundi
la waandishi wa habari.
Naye Mkuu wa
Mkoa Mwanza, John Mongella aliyekuwa mgeni rasmi kwenye hafla hiyo aliwataka
waandishi wa habari kuonyesha mwitikio mkubwa wa kujiunga na bima ya afya ya
NHIF huku wakitumia vyema wajibu wao kuelimisha wananchi kujiunga na huduma hiyo.
Awali Rais wa Muungano wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPIC), Deogratius Nsokolo alieleza kutoridhishwa na mwitikio mdogo wa waandishi wa habari ambao tayari wamejiunga na bima ya afya ya NHIF akisema kati ya 1800 waliojiunga ni 65 na wategemezi wao 20.
Klabu ya Waandishi
wa habari Mkoa Mwanza (MPC) kupitia kwa Mwenyekiti wake Edwin Soko ilitoa wazo
la waandishi wa habari nchini kujumuishwa kwenye mpango wa bima ya afya kwenye
mkutano wa wadau wa NHIF uliofanyika Disemba 2019 jijini Mwanza.
Ili
kunufaika na bima hiyo, mwandishi atapaswa kulipia shilingi laki moja na
shilingi themanini ambapo sharti kubwa ni lazima awe mwanachama wa Klabu ya
Waandishi wa Habari katika Mkoa husika hapa nchini.Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa Mwanza, Edwin Soko.
Mkurugenzi Mtendaji wa Muungano wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Abubakar Karsan (kulia) akipokea kadi ya NHIF kwenye uzinduzi wa mpango wa Bima ya Afya kwa Waandishi wa Habari.
Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella.
Wanahabari.
Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Benard Konga (kulia) pamoja na Meneja wa NHIF (kushoto) wakifuatilia hafla hiyo.
Rais wa UTPC, Deogratius Nsokolo.
Wanahabari na wadau wakifuatilia hafla hiyo.
Mkurugenzi Mkuu NHIF, Benard Konga.
Tazama BMG ONLINE TV hapa chini
SOMA>>> Matukio mbalimbali ya Wanahabari
No comments: