ILEMELA "Mabula awataka wananchi kutofanya makosa tena"
Akizungumza na mamia ya wananchi waliojitokeza katika mkutano wake wa kampeni Dkt. Mabula alisema Kata ya
Nyamanoro imekuwa nyuma kimaendeleo kutokana na wana Nyamanoro wenyewe
kumchagua diwani wa upinzani ambaye muda wote alikuwa na migogoro ya
kisiasa na wenzake na kushindwa kutatua
kero za wananchi kwa wakati.
"Ndugu zangu mkicheza mpira katika timu lazima muwe na mfumo mmoja wa mchezo, hamuwezi mkacheza mfumo wa kushambulia na wengine mfumo wa kurudi nyuma halafu mtegemee kushinda, haiwezekani na ndio maana nawaomba mniletee Maganiko (mgombea udiwani Kata ya Nyamanoro)" alisisitiza Dkt. Mabula.

Mesha aliwataka wana Nyamanoro mwaka
huu wahakikishe wanamchagua Dkt. John Pombe Magufuli upande wa urais, Dkt. Angeline Mabula upande wa ubunge na Ngaka Maganiko kwa upande wa udiwani katika Kata ya Nyamanoro.
Kwa miaka kumi Kata ya Nyamanoro ilikuwa ikiongozwa na diwani wa upinzani ambaye kwa miaka yote ya uongozi wake alikuwa akikumbana na migogoro ya kisiasa ambapo mwaka 2014 alivuliwa nafasi ya udiwani na aliyekuwa Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilemela, Henry Matata na mwaka 2015 ushindi wake ulipingwa mahakamani na aliyekuwa mgombea wa CCM, Ngaka Maganiko.
SOMA>>> Habari kutoka Ilemela
No comments: